Na AMINA KASHEBA
BONDIA Karim Mandonga ameibuka na kusema anakuja kivingine kwa kumtandika Maximilian Clavery ‘Black Cobra’katika pambano la ‘Punch ya Mama’.
Mandonga na Clavery wanatarajiwa kupanda ulingoni katika pambano la utangulizi raundi sita, uzito wa juu litakalofanyika Sikukuu ya Idd Pili katika Uwanja wa Kinesi jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam, jana, Mandonga alisema mashabiki na wadau wake wa ngumi wafike kwa wingi na wategemee ushindi mzito kutoka kwake.
“Siogopi chochote,nipo fiti nimejipanga kuhakisha napata ushindi wa kishindo, nimpatie kipigo kikali mpinzani wangu ambacho hatoweza kusahau katika miasha yake,”alisema.
Mandonga aliwaomba wadau wa ngumi kujitokeza kwa wingi katika pambano hilo, kwani amejipanga vizuri kucheza katika kiwango kikubwa.
Maximilian Clavery ‘Black Cobra’katika naye akizungumza Dar es Salaam, jana, alisema amejipanga vizuri kuhakikisha anapata ushindi wa kishindo siku hiyo.
“Nitahakikisha napata ushindi mbele ya Mandonga, sijaona sababu ya mimi kupigwa na huyo kwa sababu nimefanya mazoezi ya kutosha ili kuvunja maneno ya mpinzani wangu.
“Siku hiyo nitaonesha mchezo mzuri maana anaongea sana huyo Mandonga, nimejipanga kucheza katika kiwango kikubwa zaidi,” alisema.



