• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

RAIS YANGA AVUNJA UKIMYA KUHUSU  DAMARO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 12, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
RAIS YANGA AVUNJA UKIMYA KUHUSU  DAMARO
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS wa klabu ya Yanga Injinia Hersi Said, ameweka wazi kuhusu sakata la usajili wa kiungo wao Mohamed Damaro, akisisitiza kuwa mchezaji huyo ni Mtanzania.

Akizungumza na Shirika La Utangazaji Tanzania (TBC),Dar es Salaam, Hersi alisema leseni ya Damaro pamoja na mfumo wa usajili wa FIFA (TMS) vinamtambua kama Mtanzania.

Alifafanua usajili wa mchezaji huyo, upo sahihi na hakuna kitu kilicho tofauti na kanuni.

“Leseni ya Damaro inasoma kama mchezaji mtanzania tangu Januari 2025, sisi tukimtazama katika mfumo ambao FIFA wanautambua (TMS) mfumo unamtambua kama mchezaji wa Kitanzania, kwa hiyo sisi kama Yanga ukituingiza katika hilo sakata unatukosea.” alisema  Hersi.

Alisema mfumo wa ‘Transfer Matching System’ ni Uhamisho unaolingana na mfumo maarufu TMS ambao unamtambua Damaro kama mchezaji wa Tanzania na si raia wa Guinea.

Alisema Damaro alijiunga na Yanga, awali alikuwa anaichezea timu ya Singida Black Stars kama mchezaji wa ndani.

“Madai yanayoikosoa Yanga kuvunja taratibu za usajili hayana msingi na yanapotosha ukweli,”alisema kiongozi huyo.

Kauli hiyo, imekuja baada ya hivi karibuni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Crescentius Magori alidai kuwa wameomba kuhakiki ‘review’ kwa TFF kuhusu sakata hilo.

Alisema baada ya hapo watasonga mbele katika Mahakama ya Usuluhishi ya Michezo(CAS) na Shirikisho la Soka la Kimataifa ( FIFA).

Pia, kiongozi huyo alisema ujenzi wa uwanja, wamefikia hatua nzuri ya mchakato.

“Katika ujenzi wa uwanja tumefika kwenye eneo zuri sana. Tunafanya mchakato wetu kwa umakini mkubwa na kwa usahihi. Tuliwatangaza GSM kuwa washindi wa tenda ya ujenzi wa uwanja. Tayari tumepata mchoro wa awali wa uwanja,”alisema.

Aliongeza kuwa klabu imeshatoa maoni kuhusu mchoro huo na jana wamekamilisha michoro yote na gharama za ujenzi zote.

Kiongozi huyo alisema klabu Yanga ina wajibu wa kukuza lugha ya Kiswahili katika mchezo wa soka hapa nchini na nje ya nchi.

“Mimi na Rais wa Shirikisho la Mpira Tanzania, Wallace Karia, tunao wajibu mkubwa wa kuhakikisha lugha ya kiswahili inapenya kwa kiwango kikubwa katika medani za kimichezo za kimataifa Hususan CAF.

“Tukiwa na mshikamano madhubuti tutafanikisha lengo hili la kuweka lugha yetu hii katika daraja ambalo inastahili,” alisema Mhandisi Hersi Said.

Previous Post

 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

Next Post

DAREVA YAANIKA UMUHIMU WA AMANI

Next Post
DAREVA YAANIKA UMUHIMU WA AMANI

DAREVA YAANIKA UMUHIMU WA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA KITAIFA YA AFCON 2027

DK. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA KITAIFA YA AFCON 2027

7 months ago
VIONGOZI SIMBASC WATAKIWA KUJITATHMINI

VIONGOZI SIMBASC WATAKIWA KUJITATHMINI

9 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?