• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 16, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MAFANIKIO YA KISHINDO SGR
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI

ONGEZEKO la abiria wanaotumia Reli ya Kisasa (SGR) kufikia milioni tano ndani ya muda mfupi, limewaibua baadhi ya wadau nchini wakiwemo wachumi.

Wakizungumza na UHURU, wachumi hao walisema mafanikio hayo ni mapinduzi ya kiuchumi yanayochochewa na usafiri wa uhakika, nafuu na haraka.

Mhadhiri Mwandamizi wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Abel Kinyondo alisema uwekezaji katika miundombinu ya reli ni hatua muhimu ya kufikia azma ya kuwa kitovu cha usafirishaji Afrika Mashariki na Kati.

Alisema uboreshaji wa reli hiyo, una mchango mkubwa katika kurahisisha usafiri wa watu na mizigo.

Akizungumzia ongezeko hilo la abiria, Profesa Kinyondo alisema hali hiyo inaonesha kuna mahitaji makubwa ya huduma ya usafiri wa reli.

Alieleza reli ni njia bora ya usafiri ikilinganishwa na barabara, maji na anga, kutokana na gharama nafuu na uwezo wake wa kusafirisha haraka.

Alisema usafiri wa reli unarahisisha wananchi kufikia masoko yenye bei nzuri zaidi ya bidhaa zao, akitolea mfano wakulima wa mazao ya mahindi, alizeti na zabibu.

“Hatua hii huongeza tija katika uzalishaji na kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa, ninaishauri serikali kuongeza mabehewa ya kubeba abiria, mizigo na kuharakisha upanuzi wa reli kufikia mikoa mingine kama Mwanza na Kigoma,” alisema.

Alisema hatua hiyo itawezesha Tanzania kushindana na bandari zingine za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) Mohamed Maguo, alisema kasi ya usafiri wa SGR imekuwa kichocheo cha shughuli za kiuchumi na kijamii.

Pia imerahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa kwa muda mfupi, hivyo alishauri kuwepo takwimu za kabla na baada ya kuanzishwa usafiri huo ili kupima mchango wake katika kukuza uchumi.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa hirika la Reli Tanzania (TRC) Fred Mwanjala, alisema abiria milioni 5.5 walitumia usafiri huo kuanzia Juni, 2024.

Takwimu zilizotolewa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) zilionesha hadi Machi, mwaka huu, abiria 5,512,995 walisafiri kwa kutumia reli ya kisasa.

Alisema ongezeko hilo linaonesha SGR imejenga imani kubwa kwa watumiaji na kuwa chaguo kuu la usafiri ikilinganishwa na njia zingine.

“Mafanikio hayo yanaakisi ufanisi wa utoaji huduma, ambapo ratiba zimekuwa zikizingatiwa na uendeshaji kuwa wa kuaminika, hali inayodhihirisha uwezo wa TRC kusimamia miundombinu hiyo kwa ufanisi mkubwa.

Mwanjala alisema huduma ya SGR imeendelea kutoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii kwa kurahisisha usafiri kati ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.

Alisema mafanikio ya TRC yanaonesha uwekezaji wa serikali unaanza kuzaa matunda, ukichangia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Tangu kuanza safari za treni ya SGR hadi kufikia Machi mwaka jana, TRC iIisafirisha abiria 2,054,828 na kuwezesha kukusanya mapato ya sh. bilioni 60.2.

Previous Post

NYAMBUI AFUNGUKAAMANI KATIKA MICHEZO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

DK. MWIGULU AKERWA MICHANGO SHULENI

1 month ago
HADHI YA TANZANIA KIMATAIFA ILINDWE KWA GHARAMA ZOZOTE

HADHI YA TANZANIA KIMATAIFA ILINDWE KWA GHARAMA ZOZOTE

4 months ago

Popular News

  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYAMBUI AFUNGUKAAMANI KATIKA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?