• ePaper
Friday, April 24, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

ESPERANCE, SIMBA MECHI YA HESABU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 24, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
ESPERANCE, SIMBA MECHI YA HESABU
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

UNAWEZA kusema ni mechi ya hesabu  ambapo Simba itashuka dimba la Stade Olympique Hammadi nchini Tunisia kupambana na Esperance De Tunis.

Pambano hilo la Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi, limepangwa kuanza kufanyika saa 1:00 usiku, kocha wa timu hiyo, Steven Barker, alisema mechi hiyo ni kama fainali hivyo watapambana kuhakikisha wanapata ushindi.

Wekundu wa Msimbazi wataingia uwanjani huku wakipiga hesabu kali kuhakikisha wanachukua pointi tatu baada ya kucheza mechi mbili za michuano hiyo  na kupoteza na kusababisha kuburuza mkia katika kundi hilo.

Simba inapiga hesabu hizo, kuhakikisha inasonga mbele baada ya kupoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Stade Malien ya Mali mabao 2-1 kabla ya kupokea kichapo  kingine cha bao 1-0 kutoka kwa Petro Atletico ya Angola.

Huku Esperance nao wakipiga hesabu baada ya kucheza mechi mbili ambapo zote imetoka sare katika michuano hiyo yenye ushindani mkubwa na hivi sasa, timu hiyo ipo nafasi ya tatu katika kundi hilo.

Esperance ilianza kutoka sare ya 1-1 na timu ya Petro Atletico ya Angola na kisha ilitoka suluhu na Stade Malien katika ligi hiyo ya Mabingwa Barani Afrika hatua ya makundi.

KOCHA WA SIMBA

Akizungumza kuelekea mchezo huo, Barker alisema kuwa kila mchezo kwao ni kama fainali hivyo wataingia katika mchezo huo kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.

Alisema katika kundi lao hawajapata ushindi katika mchezo wowote ule hivyo huo ni mchezo wao muhimu wa kupata matokeo ili kujizolea pointi tatu muhimu.

“Tunaingia katika mchezo huo tukiwa tunahitaji kupata ushindi, utakuwa mchezo mgumu na wenye changamoto kubwa lakini hatutakubali kuona tunapoteza, lengo letu ni kupata pointi tatu muhimu,” alisema Barker.

Kocha huyo alisema kuwa watawaheshimu wapinzani wao kwako wapo ugenini lakini hawata waogopa kwani anaimani kubwa na kikosi chake kuwa kitafanya vizuri.

Barker alisema kuwa mashabiki na wapenzi wa timu hiyo waendelee kuipa sapoti ya kutosha timu hiyo ili iweze kufanya vizuri na kuwaongezea morari wachezaji wao ili waweze kupata matokeo mazuri.

KAULI YA WACHEZAJI

Akizungumza kwa niafa ya wachezaji wenzake wa Simba, Rushine De Reuck alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanatumia vyema mbinu walizopewa na kocha wao kupata ushindi.

 “Ni mchezo mgumu kwetu tutaingia kwa kuwaheshimu wapinzani wetu na kutafuta matokeo ya mapema, hatutakubali kupoteza, mwalimu wetu amerekebisha mapungufu yote yaliojitokeza katika mechi zilizopita,” alisema.

Rushine alisema kuwa haijalishi wapo katika uwanja wa ugenini, wamejipanga kujitoa kwa jasho na damu  kuhakikisha wanapata ushindi wa pointi tatu muhimu.

Nyota huyo alisema wachezaji wote wana morari ya kutosha kuhakikisha wanashinda mchezo huo ambao ni muhimu kwao kupata ushindi.

Ofisa Habari wa timu hiyo, Ahmed Ally alisema huo ni mchezo wa kufa au kupona hivyo wachezaji wameapa kufia uwanjani.

“Tunaomba Watanzania na wapenzi wa soka wote waweze kuiombea timu yetu ili iweze kufanya vizuri katika mchezo wetu muhimu ambao ni lazima kushinda ili tupate pointi tatu,” alisema Ahmed.

Katika mchezo wa leo, timu ya Espérance de Tunis itamkosa Nahodha wao, Yacine Meriah katika mchezo wa leo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Simba.

Yacine Meriah anakabiliwa na tatizo la misuli alilopata mapema mwezi huu.

Previous Post

MAFANIKIO YA UONGOZI WA RAIS DK. SAMIA NA HAKIKISHO LA UAMINIFU KATIKA MFUMO WA FEDHA

Next Post

MFALME WA MOROCCO ATOA NENO AFCON

Next Post
MFALME WA MOROCCO ATOA NENO AFCON

MFALME WA MOROCCO ATOA NENO AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

LEBRON JAMES NA MABADILIKO MAPYA

LEBRON JAMES NA MABADILIKO MAPYA

4 months ago
HERSI ACHOMOZA FIFA

HERSI ACHOMOZA FIFA

4 months ago

Popular News

  • MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATOA MAAGIZO ALAT

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIPOTI YA KUPONYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANDAAJI MISS WORLDTZ AITAJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?