• ePaper
Friday, April 24, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WAZIRI MKUU AWASHUKIA WACHOCHEZI MIGOGORO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 24, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WAZIRI MKUU AWASHUKIA WACHOCHEZI MIGOGORO
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Arusha

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, amewataka viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa waepuke migogoro ambayo imekuwa chanzo kwa baadhi ya miradi kukwama.

Dk. Mwigulu alitoa wito huo alipofungua Mkutano Mkuu Maalum wa Uchaguzi wa Viongozi wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) katika ukumbi wa mikutano wa AICC, jijini Arusha.

“Twendeni tukatimize wajibu wetu, tuache migawanyiko kwa sababu hayo siyo matarajio ya Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Tuepuke migogoro, mameya, madiwani na wenyeviti, kuna baadhi ya maeneo tunachelewa kutekeleza miradi ya maendeleo kwa sababu ya migogoro inayotengeneza migawanyiko.

“Ondoeni utaratibu wa kuchagua Makamu Mwenyekiti kila mwaka kwani jambo hili linaleta makovu. Nimeshamuagiza Waziri wa TAMISEMI amuandikie Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama ni sheria ifutwe, kama ni kanuni ibadilishwe, lakini kama mkutano huu una mamlaka, utaratibu wa kuchagua Makamu Mwenyekiti kila mwaka ufutwe,” alisisitiza.

Alisema utaratibu wa sasa unawanyima fursa viongozi walioko madarakani kujielekeza katika masuala ya kuwaletea maendeleo wananchi, badala yake wanajikuta katika harakati za kugawana vyeo.

“Wenyeviti wanajikuta wanaongoza watu waliogawanyika na hili halileti tija. Hivi sasa walioko madarakani bado wanajifunza kazi, tayari wengine wameshaanza kampeni kuwania nafasi zao,” alisisitiza.

Aliwataka viongozi watakaochaguliwa kesho wahakikishe wanakuwa chachu ya maendeleo na kusimamia maslahi ya wananchi kwa vitendo na kuongeza:

“Kwa viongozi mtakaochaguliwa, mhakikishe mnakwenda kusaidia jumuiya yetu na maslahi ya wananchi, muwe viongozi wanaopinga rushwa kwa vitendo. Mhakikishe mnakuwa daraja la kuleta maendeleo kwa wananchi na kuitafsiri Dira ya 2050,” alieleza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu alisema sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kufanikisha Dira ya Taifa 2050, akiwataka viongozi wa halmashauri wawe wasimamizi na walezi wa mazingira rafiki ya uwekezaji.

“Katika DIRA 2050, sekta binafsi imepewa asilimia 70 za kutoa mchango. Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri mkawe walezi wa sekta binafsi. Mkitanguliza kulea sekta binafsi mtakuza mapato. Mkitanguliza mapato mtaua sekta binafsi. Sekta binafsi tunaitegemea sana katika kutengeneza ajira kwa kinamama na vijana,” alisisitiza.

Aliwataka viongozi hao kutojihisi dhaifu katika utekelezaji majukumu yao, akisisitiza kuwa serikali inatambua mchango wao mkubwa licha ya changamoto chache zinazojitokeza.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliwahakikishia wajumbe wa mkutano kuwa serikali inaendelea kulifanyia kazi suala la kuboresha maslahi ya madiwani kama ambavyo liliwasilishwa na Mwenyekiti wa ALAT anayemaliza muda wake, Murshid Ngeze.

Previous Post

UKWELI HADHARANI TUME YA JAJI CHANDE

Next Post

4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

Next Post
4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMBA HESABU KALI, YANGA NI USHINDI TU

SIMBA HESABU KALI, YANGA NI USHINDI TU

2 months ago
CCM YAWAPONGEZA WANANCHI, YALAANI VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI

CCM YAWAPONGEZA WANANCHI, YALAANI VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI

6 months ago

Popular News

  • 4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AWASHUKIA WACHOCHEZI MIGOGORO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UKWELI HADHARANI TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YASIJIRUDIE TENA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?