Na MWANDISHI WETU
NCHI waandaji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2027 (AFCON 2027), wamesaini hati ya makubaliano ya pamoja inayojulikana kama CAF Joint Resolution – TotalEnergies AFCON PAMOJA 2027, leo Mei 11, 2026.
Nchi hizo ambazo ni Tanzania Kenya na Uganda, zimesaini hati hiyo kwa lengo la kuimarisha uratibu na ushirikiano katika maandalizi ya mashindano hayo makubwa ya barani Afrika.
Utiaji saini makubaliano hayo yameshuhudiwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dk. Patrice Motssepe.
Tanzania imewakilishwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda na Viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), wakiongozwa na Rais Wallace Karia.




