• ePaper
Wednesday, May 13, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TPA YATANGAZA KUPUNGUZA TOZO YA UENDESHAJI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 13, 2026
in Habari, Kitaifa
0
TPA YATANGAZA KUPUNGUZA TOZO YA UENDESHAJI
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imetangaza kupunguza tozo ya Uendelezaji wa Miundombinu Mipya ya Bandari (PID) kutoka asilimia tisa hadi asilimia 4.5 ya kodi ya forodha, hatua inayolenga kuongeza ushindani wa bandari za Tanzania na kutoa nafuu kwa wafanyabiashara pamoja na wadau wa usafirishaji.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa TPA, Dk George Fasha amesema uamuzi huo umetokana na maoni ya wadau wa sekta ya bandari na dhamira ya Serikali kuhakikisha biashara zinaendelea kwa mazingira rafiki.

Amesema TPA imefanya maboresho hayo baada ya kupokea maoni kutoka kwa wafanyabiashara, waingizaji na wasafirishaji wa mizigo waliotaka kiwango hicho kipitiwe upya pamoja na kuongezewa muda wa utekelezaji wake.

“Tumepunguza ada hii kutoka asilimia tisa hadi asilimia 4.5 kwa kuzingatia hali halisi ya biashara na ushauri wa wadau wetu. Mteja aliyekuwa anatakiwa kulipa shilingi laki mbili sasa atalipa laki moja,” amesema Dk. Fasha.

Kwa mujibu wa TPA, kiwango kipya kitaanza kutumika rasmi Julai Mosi, 2026.

Tozo hiyo ilianzishwa mahsusi kusaidia upatikanaji wa fedha za ujenzi na upanuzi wa miundombinu ya bandari kutokana na ongezeko kubwa la shehena nchini. Awali utekelezaji wake ulianza Machi 8, 2026 baada ya Serikali kuidhinisha marejeo ya ada za bandari za mwambao wa Bahari ya Hindi.

Baadhi ya wadau walieleza kuwa tayari walikuwa wameingia mikataba ya muda mrefu kwa kutumia viwango vya zamani vya ada, huku wengine wakitaka elimu zaidi kuhusu mfumo huo mpya.

TPA imeeleza kuwa mapato yatakayopatikana kupitia tozo hiyo yatatumika kugharimia miradi ya kimkakati ya bandari yenye thamani ya shilingi trilioni 16.1 katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa magati mapya katika Bandari ya Dar es Salaam, upanuzi wa Bandari ya Tanga, maendeleo ya Bandari ya Mtwara, ujenzi wa bandari mpya ya Kisiwa Mgao pamoja na maendeleo ya bandari kavu, matenki ya mafuta na miundombinu ya reli na barabara za kusafirisha mizigo.

Kati ya fedha zote zinazohitajika, trilioni 11.2 zinatarajiwa kupatikana kupitia mapato ya huduma za bandari huku sehemu iliyobaki ikitarajiwa kutoka kwenye ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi (PPP).

Dk Fasha alisema uwepo wa chanzo maalum cha fedha kwa ajili ya maendeleo ya bandari utawezesha utekelezaji wa miradi hiyo kwa wakati na kuongeza uwezo wa Tanzania kuhudumia nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Kwa mujibu wa takwimu za TPA, shehena inayopita katika bandari za Tanzania inatarajiwa kuongezeka kutoka tani milioni 32.8 mwaka 2024/25 hadi tani milioni 62 ifikapo mwaka 2030/31.

Katika miezi tisa ya mwaka wa fedha 2025/26 pekee, bandari zote nchini zilihudumia tani milioni 29.6 za shehena pamoja na makasha zaidi ya milioni moja kwa mara ya kwanza katika historia ya sekta hiyo nchini.

Previous Post

POINTI UBINGWA YANGA SC KUSAKWA LEO

Next Post

BALOZI DK. BASHIRU AONGOZA JUMUIKO LA KADEFO AKITAJA JITIHADA ZA RAIS DK. SAMIA KUENDELEZA KAGERA

Next Post
BALOZI DK. BASHIRU AONGOZA JUMUIKO LA KADEFO AKITAJA JITIHADA ZA RAIS DK. SAMIA KUENDELEZA KAGERA

BALOZI DK. BASHIRU AONGOZA JUMUIKO LA KADEFO AKITAJA JITIHADA ZA RAIS DK. SAMIA KUENDELEZA KAGERA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA

SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA

6 months ago
ZANZIBAR YANG’ARA KIMATAIFA

ZANZIBAR YANG’ARA KIMATAIFA

5 months ago

Popular News

  • BEHEWA LA AFYA LAIBUA WADAU

    BEHEWA LA AFYA LAIBUA WADAU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • IDADI WAGONJWA AFYA YA AKILI TISHIO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BALOZI DK. BASHIRU AONGOZA JUMUIKO LA KADEFO AKITAJA JITIHADA ZA RAIS DK. SAMIA KUENDELEZA KAGERA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TPA YATANGAZA KUPUNGUZA TOZO YA UENDESHAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • POINTI UBINGWA YANGA SC KUSAKWA LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?