• ePaper
Monday, May 25, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MAKONDA ASISITIZA KULINDWA KWA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA CHINA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 25, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MAKONDA ASISITIZA KULINDWA KWA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA CHINA
0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema Tanzania itaendelea kuimarisha na kulinda ushirikiano wake na China, akieleza kuwa utamaduni umeendelea kuwa daraja muhimu la kuunganisha mataifa hayo mawili.

Makonda alisema hayo katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mazungumzo kati ya Tamaduni yaliyofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam.

Alisema Tanzania na China zimeendelea kushirikiana katika maeneo mbalimbali ikiwemo sanaa, utamaduni, elimu pamoja na diplomasia ya watu kwa watu.

“Utamaduni umeendelea kuwa kiungo muhimu cha urafiki na mshikamano wetu,” alisema Makonda.

Aidha, alisema mafanikio mengi yaliyofikiwa kupitia ushirikiano huo yanaonesha namna mahusiano ya kihistoria kati ya mataifa hayo yalivyoendelea kuimarika.

Makonda alitaja mradi wa TAZARA Railway Construction kuwa moja ya alama kubwa za ushirikiano huo pamoja na mchango wa China katika harakati za ukombozi wa Afrika.

“Miradi mikubwa kama Reli ya TAZARA ni ushahidi wa urafiki wa muda mrefu kati ya Tanzania na China,” alisema.

Pia alisema Serikali imeanza ujenzi wa Kituo Kikuu cha Kisasa cha Uhifadhi wa Historia ya Ukombozi wa Afrika katika eneo la Kongwa mkoani Dodoma kwa ajili ya kuhifadhi kumbukumbu muhimu za harakati za ukombozi wa bara hilo.

Maadhimisho hayo yaliambatana na maonesho ya sanaa na ngoma za asili kutoka Tanzania na China.

Kwa upande wake, Chen Mingjian alisema mwaka huu ni mwaka wa mabadilishano ya watu kwa watu kati ya China na Afrika pamoja na maadhimisho ya miaka 70 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Afrika.

Alisema urafiki wa Tanzania na China umejengwa tangu zamani kupitia mshikamano na ushirikiano wa maendeleo ikiwemo kipindi cha ujenzi wa Reli ya TAZARA.

Previous Post

WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

Next Post

TUCTA YATAKA WAANDISHI KUHAMASISHA WAAJIRI KURIPOTI MATUKIO WCF

Next Post
TUCTA YATAKA WAANDISHI KUHAMASISHA WAAJIRI KURIPOTI MATUKIO WCF

TUCTA YATAKA WAANDISHI KUHAMASISHA WAAJIRI KURIPOTI MATUKIO WCF

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MATARAJIO YA WASOMI TUME YA JAJI CHANDE

MATARAJIO YA WASOMI TUME YA JAJI CHANDE

2 months ago
UTEKELEZAJI ILANI UNVYOCHOCHEA MAGEUZI SEKTA YA AFYA UVINZA

UTEKELEZAJI ILANI UNVYOCHOCHEA MAGEUZI SEKTA YA AFYA UVINZA

3 months ago

Popular News

  • MWIGULU AKERWA WANAOPORA HAKI

    MWIGULU AKERWA WANAOPORA HAKI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA YATAKA WAANDISHI KUHAMASISHA WAAJIRI KURIPOTI MATUKIO WCF

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAKONDA ASISITIZA KULINDWA KWA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA CHINA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?