Na AMINA KASHEBA
RATIBA ngumu ya Ligi Kuu Tanzania Bara imetajwa kuwa sababu ya Simba kutopata matokeo mazuri, waliyotarajia katika mchezo dhidi ya Dodoma Jiji.
Simba iliumana na Dodoma Jiji juzi, katika mechi iliyopigwa Uwanja wa KMC Complex , Mwenge jijini Dar es Salaam. ilishinda 1-0 na kuvuna alama tatu.
Katika pambano hilo, bao la ushindi lilifungwa na Elie Mpanzu dakika ya 63.
Akizungumza baada ya kumaliza mchezo huo, Barker alisema timu yake imekuwa na ratiba ngumu ya kucheza, hali ambayo inasababisha kutopata ushindi mnono.
“Hii ni mechi ya 16 ndani ya siku 52, si jambo zuri kwa wachezaji maana wanakosa muda wa kupumzika” alisema kocha, mechi zimekuwa nyingi sana,” alilalama kocha.
Kocha huyo alisema uwepo wa mechi za timu ya taifa katika kalenda ya Shirkisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), utatoa nafasi ya wachezaji wake kupumzika na kufanya maandalizi mazuri kwa michezo iliyobaki.
Kocha wa Dodoma Jiji, Amani Josiah alisema amefurahi kuona mpango kazi wake umeleta ushindani katika mechi yao dhidi ya Simba.
‘Mechi ilikuwa na ushindani mkubwa, nawapongeza wachezaji wangu kwani wamefuata yale niliyowaelekeza, nimefurahishwa na kiwango cha kipa wangu, Daniel Mgore,” alisema Josiah.



