• ePaper
Thursday, June 4, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

admin by admin
June 1, 2026
in Burudani, Michezo
0
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa imesimama kupisha mechi za kirafiki za kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), timu za Simba na Yanga zimeweka wazi kwamba zinaendelea na kazi ya maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Yanga itakuwa ugenini dhidi ya Mashujaa FC, Juni 13, mwaka huu huku Simba wakibaki nyumbani kupambana na Pamba Jiji Juni 14, mwaka huu katika mchezo wa mzunguko wa 26 wa ligi hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema baada ya mapumziko mafupi kikosi chao kitaendelea na maandalizi kwa ajili ya mechi tano zilizobakia.

“Wale wachezaji wetu abao hawakuitwa katika timu za taifa, wataingia kambini Juni Mosi, mwaka huu kwa ajili ya maandalizi ya mechi zilizobakia, na baada ya hapo watakuja kuungana na wale walioitwa katika kikosi cha taifa ili kuendeleza programu ya mwalimu wetu,” alisema.

Kamwe alifafanua kuwa wanaendelea  kujiandaa na mchezo dhidi ya Mashujaa wakijua ni mchezo mgumu na wenye changamoto kubwa.

Aliongeza kuwa mechi tano za mwisho, zinahitaji maandalizi ya kutosha kuhakikisha wanapata ushindi na kutetea ubingwa wao.

Naye Meneja wa Habari na Mawasilino Simba, Ahmed Ally alisema kocha wao, Steve Barker amewapa mapumziko wachezaji wao.

Ahmed alisema wanajua mechi za mwisho wa msimu zinakuwa ngumu na zenye changamoto kubwa lakini hawatakubali kupoteza mchezo wowote ule.

“Unajua mechi za mwisho wa msimu zinakuwa ngumu na zenye changamoto kubwa lakini anaimani wachezaji wetu watapambana mwanzo mwisho ili kupata pointi tatu katika kila mchezo,” alisema Ahmed.

Alisema kuanzia Juni mosi, timu itaanza kufanya maandalizi katika mchezo wake dhidi ya Pamba Jiji.

Katika msimamo wa ligi, Yanga inaongoza ikiwa na pointi 60 huku Simba ikishika nafasi ya pili ikiwa na pointi 58 baada ya wote kushuka dimbani mara 25.

Timu hizo zimebakiza mechi tano ili kumaliza ligi kuu msimu huu, Yanga ikibakiwa na mchezo dhidi ya Mashujaa FC, Fountain Gate FC, Azam FC, TRA United na JKT Tanzania.

Kwa upande wa Simba imebakiwa na michezo dhidi ya Pamba Jiji, Mbeya City, Mtibwa Sugar, Singida Black Stars na KMC.

Previous Post

SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

Next Post

ASANTE SERENGETI BOYS

Next Post
ASANTE SERENGETI BOYS

ASANTE SERENGETI BOYS

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NI MWANZO WA SIMULIZI MPYA

NI MWANZO WA SIMULIZI MPYA

5 months ago
MATOKEO YA DARASA LA SABA YATANGAZWA

MATOKEO YA DARASA LA SABA YATANGAZWA

7 months ago

Popular News

  • TANZANIA, RUSSIA KUPAISHA UCHUMI

    TANZANIA, RUSSIA KUPAISHA UCHUMI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ASANTE SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?