• ePaper
Wednesday, June 10, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 7, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

TIMU za Simba na Yanga zimetoa msimamo kwamba zipo tayari muda wowote kuendelea na mechi zao tano za Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ligi Kuu Tanzania ilisimama kwa muda kupisha mechi za Kimataifa za kirafiki ambazo zilitakiwa kucheza Juni 5 na Juni 9, mwaka huu nchini Morocco ambazo kwa sasa zimefutwa

Awali Taifa Stars ilipangwa  kuchezaJuni 5, mwaka huu na Uganda kabla ya kuibakibili Rwanda, Juni 9, mwaka huu mechi zote zilipangwa kuchezwa jijini Marrakech nchini Morocco na kurejea tena Juni 12, mwaka huu.

Baada ya kuondolewa kwa mechi hizo, Kaimu Ofisa Habari wa TPLB, Yahya Abushehe alisema baada ya mechi hizo kufutwa Bodi itatangaza tena ratiba mpya.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema wamejipanga muda wowote kurejea uwanjani kwa ajili ya ligi hiyo yenye ushindani mkubwa.

Alisema timu yao tayari ilikuwa katika mandalizi ya mechi zinazofuata.

“Tunajua zile mechi za timu ya Taifa hazichezwi tena na wachezaji watarajea, hivyo sisi kama klabu tupo tayari kwa mapambano muda wowote,” alisema Ahmed.

Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema hawana wasiwasi na wanapenda michuano hiyo iendelee kuchezwa.

“Timu yetu ipo tayari muda wowote ule kwa ajili ya kupambana na kupata matokeo mazuri, sisi hatuna hofu yeyote tunasubiri kama kutakuwa na mabadiliko yeyote ya ratiba basi tupo tayari kwa ajili ya mapambano,” alisema.

Kamwe alisema kila mchezaji anapenda kuitumikia timu kuhakikisha ushindi unapatikana.

Naye Mkuu wa idara ya Habari na Mawasiliano, Azam FC, Zacharia Thabit ‘Zaka’, alisema timu yao inaendelea na mazoezi na wamejipanga muda wowote kushuka dimbani.

“Sisi tumejipanga muda wowote kushuka dimbani kwa ajili ya kupambana na mechi zetu tano zilizobakia hivyo kila mchezaji anajua nini anatakiwa kufanya na tupo tayari kurejea uwanjani,” alisema Zaka.

Hadi sasa Yanga ikibaki na mchezo dhidi ya Mashujaa FC, Fountain Gate FC, Azam FC, TRA United na JKT Tanzania.

Simba yenyewe imebaki na mechi dhidi ya Pamba Jiji, Mbeya City, Mtibwa Sugar, Singida Black Stars na KMC huku Azam wao wakibaki na mchezo dhidi ya Fountain Gate, Mashujaa, Yanga, Coastal Union na Dodoma Jiji.

Yanga inaongoza ligi hiyo, ikiwa na pointi 60 ikifuatiwa na Simba yenye alama 58 huku Azam ikishika nafasi ya tatu, ina pointi 52.

Previous Post

MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

Next Post

WASOMI WADOKEZA MANUFAA YA UWEKEZAJI MAENEO MANNE

Next Post
WASOMI WADOKEZA MANUFAA YA UWEKEZAJI MAENEO MANNE

WASOMI WADOKEZA MANUFAA YA UWEKEZAJI MAENEO MANNE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ASISITIZA VIJANA KULINDA AMANI

DK. SAMIA ASISITIZA VIJANA KULINDA AMANI

8 months ago
KOCHA GABON AITAKANUSU FAINALI

KOCHA GABON AITAKANUSU FAINALI

6 months ago

Popular News

  • WASOMI WADOKEZA MANUFAA YA UWEKEZAJI MAENEO MANNE

    WASOMI WADOKEZA MANUFAA YA UWEKEZAJI MAENEO MANNE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?