• ePaper
Monday, May 25, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

JUKWAA LA WANAWAKE LAIBUKA  NA MAAZIMIO 10 KUHUSU AMANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 5, 2025
in Habari, Kitaifa
0
JUKWAA LA WANAWAKE LAIBUKA  NA MAAZIMIO 10 KUHUSU AMANI
0
SHARES
18
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Dodoma
NA MWANDISHI WETU

JUKWAA la Wanawake Tanzania limeazimia mambo 10 yenye lengo la kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu kuilinda amani iliyopo huku likimpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kurejesha utulivu nchini.

Maazimio hayo yametolewa jijini hapa na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Zainab Shomari katika kongamano la Jukwaa la Wanawake 2025.

Amesema azimio la kwanza ni jukwaa hilo kuendelea kuwa sehemu ya ujenzi wa amani ya kudumu kwa kuimarisha majadiliano na maridhiano yenye kujenga jamii kwani mazungumzo ya wazi ndiyo uimarisha mshikamano.

Pia, amesema azimio la tatu ni kuendeleza matumizi salama yenye uadilifu ya mitandao ya kidijitali kwa kutumia maudhui yenye kukuza umoja, kuheshimiana, ustaarabu na kutunza taswira ya Taifa.

Azimio la nne lililofikiwa katika jukwaa hilo lililowakutanisha washiriki zaidi ya 2000 ni kuhamasisha, kuongeza fursa za maendeleo kwa wanawake na vijana katika maeneo mbalimbali ya jamii.

“Azimio la tano ni kujizatiti katika kuelimisha jamii yetu kuhusu maadili, utu, uzalendo na utatuzi wa migogoro kwa njia za hekima kwa kuwa hivi ndivyo vinavyoijenga Tanzania kuwa taifa linalosikilizana, kuvumiliana na linaloheshimu umoja wetu.

“Tukiwa nguzo ya malezi, tuna wajibu wa kuandaa vizazi vinavyothamini amani kama sehemu ya utambulisho wa taifa letu,” alisema Shomari.

Amesema azimio la sita ni kukubali wajibu wao katika kutimiza ndoto ya Tanzania waitakayo kwani Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, imeweka bayana kwamba amani ni msingi wa uchumi jumuishi na shindani.

Vilevile, amesema azimio la sita ni kujitolea kwa dhati kushiriki kikamilifu kuilinda na kuiendeleza amani kwa vitendo.

Pia, katika azimio la saba kongamano hilo lilimpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa hatua zote alizochukua kurejesha hali ya amani na utulivu nchini.

Zainab amesema azimio la nane ni kuunga mkono uteuzi wa Tume ya Uchunguzi ili kuweka mazingira mazuri ya kuwepo maridhiano na maelewano nchini.

Azimio la tisa ambalo kongamano hilo lilikuja nalo ni kwamba wanawake nchini wataendelea kuwa sehemu muhimu ya ustawi wa taifa kwa kuzingatia hekima, utulivu na umoja.

“Tunatoa neno la faraja kuonesha mshikamano na wote ambao walipitia kadhia hiyo.  Tukiwa sauti ya amani, tunathamini utulivu na tunaunga mkono hatua ya Rais Dk. Samia kuunda Tume ya Uchunguzi kwa lengo la kupata ukweli, kuweka misingi ya maelewano na kuimarisha umoja wa taifa,” amebainisha.

Katika azimio la kumi, kongamano hilo lilitoa wito kwa Watanzania hususan vijana kuhakikisha wanaendelea kudumisha amani na kujenga mazingira ya kutumia mazungumzo, majadiliano na maridhiano.

Previous Post

IBENGE ALIA NA WASHAMBULIAJI

Next Post

VIJANA LINDENI AMANI YA NCHI – DK. MIGIRO

Next Post
VIJANA LINDENI AMANI YA NCHI – DK. MIGIRO

VIJANA LINDENI AMANI YA NCHI - DK. MIGIRO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TUNAMWOMBEA KURA DK. SAMIA, WATANZANIA NI MASHAHIDI – WASIRA

TUNAMWOMBEA KURA DK. SAMIA, WATANZANIA NI MASHAHIDI – WASIRA

9 months ago
KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI

KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI

2 days ago

Popular News

  • WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA KIHONGOSI YAACHA NEEMA KWA WANAWAKE MARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YAJIPANGA KUDHIBITI MIJI HOLELA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?