Na Mwandishi Wetu
WAKAZI wawili wa Kinyerezi, Dar es Salaam, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na shtaka la unyang’anyi wa kutumia silaha kisha kujipatia vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh. bilioni 1.5
Washitakiwa hao ni Tumaini Moshi (33) na Gaspar Mmari (24) ambapo walifikishwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya.
Akiwasomea shtaka hilo, Wakili wa Serikali, Frank Rimoy alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya jinai namba 28915/2025 ambalo ni shtaka la unyang’anyi wa kutumia mawe, fimbo na nondo ili kujipatia vitu hivyo.
Ilidaiwa kuwa washitakiwa walitenda kosa hilo Oktoba 29 mwaka huu katika Klabu ya The Voice Tz Limited iliyopo Kinyerezi ambapo walifanya unyang’anyi kwa kutumia silaha kisha kuiba vitu vilivvokuwepo ndani va klabu hivo.
Wakili Rimoy alidai kuwa wakiwa katika eneo hilo waliiba viti 350 vya mbao na plastiki vyenye thamani ya sh. Milioni 150, vifaa vya ofisini wenve thamani va sh. milioni 40 na runinga 57 zilizokuwa na thamani ya sh. milioni 480.
Pia, inadaiwa washitakiwa hao waliiba seti ya muziki yenye thamani ya sh. milioni 250, mshine ya mfumo wa malipo (POS) yenye thamani ya sh. milioni 80 na vyombo wa iikoni wa thamani va sh.milioni 25.
Kadhalika, ilidaiwa waliiba vifaa wa baa yenye thamani ya sh. milioni 15 vinywaji mbalimbali vyenye thamani ya sh. milioni 518 na fedha taslimu kiasi cha sh.
milioni 16.9.
Washitakiwa hao ilidaiwa kabla na baada ya wizi huo waliwatishia Jammy Galus, Masoud Ahmed na Benedict Katarunga kwa kutumia mawe, fimbo na nondo.
Baada ya maelezo hayo, Wakili Rimoy alidai upelelezi wa haujakamilika, hivyo aliomba tarehe nyingine ya kutajwa.
Hakimu Lyamuya, aliahirísha kesi hiyo hadi Desemba 22 mwaka huu kwa kútajwa, hivyo washitakiwa walirudishwa rumande kwani shtaka la unyang’anyi wa kutumia silaha halina dhamana kwa mujibu wa sheria.




