• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MAHAKAMA ZANUFAIKA NA MAGEUZI YA TEHAMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 15, 2025
in Habari, Kitaifa
0
MAHAKAMA ZANUFAIKA NA MAGEUZI YA TEHAMA

WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Happiness Mtweve
Dodoma

SERIKALI imesema imeshuhudia mapinduzi makubwa katika taasisi zinazohusika na utoaji wa haki baada ya kuanza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika Mahakama na Mabaraza ya Haki, hatua iliyochangia kuharakisha uendeshaji wa mashauri na kuongeza ufanisi katika utoaji wa haki.

Aidha, Serikali imesema kuwa chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kusisitiza utekelezaji wa mageuzi ya kidijitali kama nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa na uboreshaji wa huduma kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dodoma leo Desemba 15, 2025 na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya TEHAMA kwa taasisi mbalimbali za kisheria.

Vifaa hivyo ni pamoja na kompyuta mpakato 70 na mashine za kuchapisha (printers) zilizogawiwa kwa Wizara ya Katiba na Sheria (10), Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (20), Ofisi ya Mashtaka ya Taifa (20) pamoja na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Mahakama (20).

Waziri Kairuki amesema matumizi ya TEHAMA yameondoa urasimu, yameimarisha mifumo ya kazi, kupunguza msongamano wa mashauri na kuondoa mianya ya rushwa kwa watumishi wasio waaminifu.

Ameongeza kuwa teknolojia hiyo imewezesha pia kukubalika kwa ushahidi wa kielektroniki na kurahisisha tathmini ya utendaji wa Mahakama na watendaji wake.

“Hatua hizi zimewezekana kwa kiasi kikubwa kutokana na mchango wa Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kutunga sera na sheria zinazowezesha utoaji wa haki kwa kutumia TEHAMA,” amesema Waziri Kairuki.

Ameitaja miongoni mwa sheria hizo kuwa ni Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Sheria ya Miamala ya Kielektroniki ya mwaka 2015 pamoja na Sheria ya Ushahidi ya mwaka 2002 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2007.

Previous Post

TANZANIA REJEA YA AMANI – UN

Next Post

MAADILI KAZINI YAWE MSINGI WA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI – NDEJEMBI

Next Post
MAADILI KAZINI YAWE MSINGI WA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI – NDEJEMBI

MAADILI KAZINI YAWE MSINGI WA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI – NDEJEMBI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

6 months ago
RAIS DK. SAMIA KUONGOZA SHUGHULI YA KUMUAGA LUKUVI DAR

RAIS DK. SAMIA KUONGOZA SHUGHULI YA KUMUAGA LUKUVI DAR

3 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?