• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MBIO ZA UBINGWA LIGI KUU ENGLAND KATIKA KRISIMASI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 22, 2025
in Burudani, Michezo
0
MBIO ZA UBINGWA LIGI KUU ENGLAND KATIKA KRISIMASI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

LONDON, England

ARSENAL ya Mikel Arteta itasherehekea Sikukuu ya Krisimasi mwaka huu ikiwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL).

Wakati michuano hiyo ikielewa katikati mwa msimu, nini maana ya kuongoza ligi katika sikukuu hiyo hususan katika mbio za ubingwa?

Sikukuu ya Krisimasi husherehekewa Desemba 25 ya kila mwaka ikimaanisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.

Katika msimamo huo, Arsenal ndiyo kinara ikiwa na pointi 39 katika mechi 17 wakati Man City ikiwa nafasi ya pili kwa alama 37 baada ya kucheza mechi 37.

MBIO ZA UBINGWA

Timu ambayo huwa kileleni mwa msimamo katika Sikukuu ya Krisimasi mara nyingi huwa bingwa wa msimu husika, japokuwa siyo mara zote.

Katika misimu 33 iliyopita, timu 17 zilizoongoza ligi katika sikukuu hiyo, zilitwaa taji katika msimu huo.

Hata hivyo, Arsenal yenyewe imeshindwa kunufaika na jambo hilo kwani awali imeshakuwa kileleni mwa msimamo mara nne wakati wa Krisimasi lakini haijatwaa ubingwa.

Katika misimu 33 iliyopita, Man United (7) na Chelsea (5) ndizo timu zinazoongoza kwa kutwaa taji hilo mara nyingi (5) baada ya kuwa kileleni mwa msimamo katika Krisimasi wakati Liverpool ikifuatia kwa kutwaa mara mbili katika Krisimasi saba.

Kabla ya Mikel Arteta kuichukua timu hiyo, Arsenal iliwahi kuongoza katika Krisimasi mara mbili, lakini sasa ni mara ya tatu katika misimu minne ‘The Gunners’ inaongoza ligi Krisimasi.

Mashabiki wa Arsenal wanaamini kwamba kwa mara zote ambazo Arsenal imeongoza ligi katika Krisimasi na kushindwa kutwaa taji, basi imetosha na sasa Arteta ana kila sababu ya kuipa miamba hiyo kombe la kwanza la EPL ndani ya miaka 21.

ARSENAL INAWEZA KUFIKA MBALI?

Hakupaswi kuwa na sehemu yoyote ya kufanya makosa kwani miamba hiyo kutoka London hivi sasa inaongoza ligi kwa utofauti wa alama mbili pekee dhidi ya Man City wakati wastani wa timu bingwa kuongoza ligi katika Krisimasi ni pointi nne.

Kwa mujibu wa mchanganuo huo, timu pekee ambayo imeongoza ligi kwa alama chache katika Krisimasi ndani ya misimu 12 iliyopita ni Arsenal miaka miwili iliyopita.

Hata hivyo, Arsenal ndiyo timu pekee kushinda taji la EPL bila ya kufanya hivyo wakati inaongoza ligi katika Krisimasi, ambapo mataji yake yote matatu yaliyopita miamba hiyo haikuwa kinara katika Krisimasi.

Miamba hiyo iliwahi kuwa nyuma kwa alama 13 dhidi ya kinara Man United na ikaenda kutwaa taji la EPL msimu wa 1997/1998.

Pia, miamba hiyo ilikuwa nyuma pointi mbili dhidi ya Newcastle mwaka 2001/2002 na ikaenda kutwaa taji kabla ya kuwa nyuma kwa alama tatu dhidi ya Man United msimu wa 2003/2004 na ikaenda kubeba taji.

Arsenal itakuwa ya tofauti msimu huu?

Mashabiki wengi wa Arsenal wamezoea kuishuhudia timu yao ikiwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu England katika Krisimasi na baadaye kukosa taji hususan dhidi ya Man City ya Pep Guardiola.

“Tumerejea kileleni mwa msimamo lakini hatuitazami sana Man City au timu nyingine.,” alisema nyota wa Arsenal, Bukayo Saka.

Arteta alisema: “Tupo kileleni sasa, tunajua kama tutashinda kila wiki tutakaa palepale. Kitu pekee tunachoweza kilichopo katika uwezo wetu ni kiwango chetu binafsi na matokeo na tunajua ni kwa kiasi gani ligi ni ndefu na ngumu,”.

Hata hivyo, Kocha Pep Guardiola, alisema timu yake itaendelea kuwepo katika mbio za ubingwa huku akikisisitiza wanahitaji kuwa bora zaidi.

Previous Post

AFCON 2025 KINAWAKA KATIKA VIWANJA HIVI

Next Post

STARS IFANYE NINI KUTOBOA AFCON?

Next Post
STARS IFANYE NINI KUTOBOA AFCON?

STARS IFANYE NINI KUTOBOA AFCON?

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAPANDISHWA KIZIMBANI WAKIDAIWA KUIBA MALI ZA SH. BILIONI 1.5

WAPANDISHWA KIZIMBANI WAKIDAIWA KUIBA MALI ZA SH. BILIONI 1.5

4 months ago
NYOTA YANGA WAPEWA TANO

NYOTA YANGA WAPEWA TANO

6 days ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?