• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI YATOA MILIONI 800/- UJENZI KITUO CHA POLISI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 26, 2025
in Habari, Kitaifa
0
SERIKALI YATOA MILIONI 800/- UJENZI KITUO CHA POLISI
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Morogoro
NA LATIFA GANZEL

SERIKALI imetoa zaidi ya sh. milioni 800 kukamilisha ujenzi Kituo cha Polisi ngazi ya daraja B kilichopo Ifakara wilayani  Kilombero mkoani Morogoro.

Akiweka jiwe la msingi katika kituo hicho kilichokamilika kwa zaidi ya asilimia 95, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Dustan Kyoba, alisema fedha hizo ni matokeo ya juhudi za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha wananchi wanaishi kwa usalama.

Wakili Kyoba alitoa shukran kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camillus Wambura kwa kuungana na serikali kuchangia sh. milioni 32 kukamilisha mifumo ya Tehama katika kituo hicho.

Kyoba alisisitiza upandaji miti katika maeneo yanayozunguka kituo hicho na kuwekeza nguvu kuzuia uhalifu mtandaoni.

Kwa upande wake, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Samuel Kijanga, alimshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa kuhamasisha ujenzi huo.

Naye, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kilombero, SSP David Nkuba, alisema kituo hicho kimejengwa kwa ‘forced account’ ukisimamiwa na mkandarasi wa ndani.

Akizungumzia ujenzi huo, mkazi wa eneo hilo Laison Makwalilo alisema uwepo wa kituo hicho kitawezesha kupungua uhalifu katika wilaya hiyo.

Wakati huo huo, watu 14 wakiwemo wanaume 11 na wanawake watatu wamenusurika kifo katika ajali ya basi na lori iliyotokea juzi katika eneo la Magubike, Kata ya Magubike, Wilaya ya Kilosa barabara ya Morogoro-Dodoma huku chanzo cha ajali hiyo kikitajwa ni uzembe wa dereva wa basi

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Alex Mkama, alisema ajali hiyo ilihusisha magari mawili yaliyogongana uso kwa uso ambapo gari la kwanza ni basi lenye namba za usajili T 577 DXL aina ya Yutong, mali ya Kampuni ya NASRI  likiendeshwa na Alex Patric (40) mkazi wa Milandizi mkoani Pwani, likitokea Tarime kwenda Dar es Salaam.

Alisema gari la pili ni lori aina ya Scania lenye namba za usajili T 145 AFA  na tela lenye namba T 148 AFK, mali ya Kampuni ya ATT, likiendeshwa na Robert Manunu (30) mkazi wa Bariadi mkoani Simiyu likitokea Morogoro kwenda mkoani Tabora.

Majeruhi wa ajali hiyo walifikishwa katika Kituo cha Afya Magubike kupatiwa matibabu ambapo uchunguzi wa awali ulibaini chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa basi aliyetaka kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari. Kamanda huyo alisema dereva huyo wa basi anapatiwa matibabu chini ya ulinzi Jeshi la Polisi ili hatua zaidi za kisheria zichukuliwe.

Previous Post

JELA MIAKA 25 KWA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

Next Post

RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

Next Post
RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI

WAKUU WA VYOMBO VYA HABARI NA WAHARIRI WAANDAMIZI NCHINI, WATOA MAAZIMIO WATANZANIA KUTUNZA AMANI

6 months ago
DK. SAMIA AWAPA FARAJA WENYE MAHITAJI MAALUMU

DK. SAMIA AWAPA FARAJA WENYE MAHITAJI MAALUMU

6 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?