• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA QUEENS MENO NJE, YANGA YALIA NA WACHEZAJI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 30, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA QUEENS MENO NJE, YANGA YALIA NA WACHEZAJI
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

WAKATI timu ya Simba Queens ikifurahia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga Princess, wapinzani wake hao wamelia na makosa madogo yaliyofanywa na wachezaji wake.

Simba Queens ilipata ushindi huo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara uliopigwa katika Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam, Kocha wa Simba Queens, Mussa Hassan ‘Mgosi’, alisema ubora na utulivu wa wachezaji wake ndiyo sababu ya kuvuna pointi tatu muhimu.

“Niwapongeze wachezaji wangu, walifuata kile tulichofanya katika uwanja wa mazoezi. Ili uwe bingwa unapaswa kuzifunga timu bora na kupata ushindi katika kila mchezo, ikishindikana sana basi hata sare,” alisema.

Kocha huyo alisema kikosi chake kilikuwa bora kimbinu zaidi wa wapinzani wake hatua ambayo pia iliwaongoza kupata ushindi huo.

Naye Kocha wa Yanga Princess, Edna Lema alisema kilichosababisha hadi kufungwa ni wachezaji wake kufanya makosa ambayo wapinzani wao waliyatumia na kupata ushindi.

“Makosa madogo madogo yamesababisha hadi kupoteza mchezo kwani wachezaji wangu hawakuwa makini, lakini niwapongeze kwa kuonyesha ushindani mbele ya mtani kwa sababu mechi ilikuwa ngumu,” alisema..

Kutokana na matokeo hayo, Simba Queens ipo kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara ikiwa na pointi 15 wakati Yanga Princess ikiwa nafasi ya tatu kwa alama 12, zote zikicheza mechi tano.

Previous Post

TAKWIMU ZAMBEBA MNIGERIA ALIYEKANDWA NA MWAKINYO

Next Post

MAJIHA APANIA KUTETEA MKANDA WBO AFRIKA

Next Post
MAJIHA APANIA KUTETEA MKANDA WBO AFRIKA

MAJIHA APANIA KUTETEA MKANDA WBO AFRIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AAHIDI FURSA ZAIDI KWA VIJANA NCHINI

DK. SAMIA AAHIDI FURSA ZAIDI KWA VIJANA NCHINI

7 months ago
DRC WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUTOA HIFADHI YA WAKIMBIZI

DRC WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUTOA HIFADHI YA WAKIMBIZI

3 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?