• ePaper
Wednesday, April 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 11, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto mchanga wa kike leo tarehe 11 Machi, 2026, katika makazi yake, Ikulu Chamwino, jijini Dodoma.

Mtoto huyo aliyepewa jina la Grace Samia Suluhu, alitelekezwa mjini Nzega, mkoani Tabora, amekabidhiwa kwa Rais Dk. Samia.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mtoto huyo, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitapwaki Tukai, amesema mtoto huyo aliokotwa  Januari 17, 2026 akiwa ametelekezwa katika jirani na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega mjini.

Amesema alipopata taarifa hizo alishirikiana na jeshi la polisi kumchukua  na kumpeleka hospitalini kwa uchunguzi na uangalizi, huku juhudi za kumtafuta mama yake zikiendelea bila mafanikio.

Rais Dk. Samia amemkaribisha mtoto huyo katika familia yake na kuahidi kumpa malezi, ulinzi na huduma zote muhimu ili akue katika mazingira salama na yenye upendo.

“Wanaotupa watoto hawajui wanalolifanya. Kuliko kumtupa mtoto ni afadhali ukamkabidhi katika mamlaka za kisheria au kituo cha kulelea watoto. Kila mtoto aliyezaliwa ni hazina na hatuijui kesho yake,” amesema Rais Dk. Samia.

Previous Post

SINGIDA, SIMBA BALAA ZITO LEO

Next Post

MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

Next Post
MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MADHARA YA MVUA

MADHARA YA MVUA

4 months ago
MABAO 104 YAFUNGWA LIGI KUU BARA

MABAO 104 YAFUNGWA LIGI KUU BARA

5 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?