• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WAZIRI MKUU AWAPA ‘TANO’ WANAOCHAPAKAZI SERIKALINI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 9, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WAZIRI MKUU AWAPA ‘TANO’ WANAOCHAPAKAZI SERIKALINI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema serikali inatambua uwepo wa watumishi wa umma wanaofanya kazi vizuri.

Dk. Mwigulu aliwataka watumishi waadilifu kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na kujiepusha kujiingiza katika makundi ya wazembe, wezi na wanaofanya kazi kwa mazoea.

“Serikali haitomuonea mtu, watumishi wachapakazi wasiingie ubaridi kwa sababu serikali inatambua mchango wao katika maendeleo ya taifa. Watu wasome alama za nyakati serikali haitovumilia masuala ya wizi kwa sababu yanarudisha nyuma maendeleo,” alisema.

Dk. Mwigulu alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Namanyere wilayani Nkasi mkoani Rukwa.

Aliwasisitiza watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na kuepuka udokozi kwa sababu haukubaliki na hauvimiliki.

Waziri Mkuu aliwataka watumishi wa umma watekeleze majukumu yao kwa kusimamia ipasavyo ujenzi wa miradi.

UCHIMBAJI VISIMA

Pia, alisisitiza mikoa yote kuhakikisha katika upangaji wa bajeti, wanaweka vipaumbele vya uchimbaji visima kupitia mitambo iliyosambazwa katika mikoa yao.

“Mitambo ya uchimbaji maji itumike kuchimba visima wananchi wapate maji ya uhakika,” alisema Dk. Mwigulu.

Aidha, alizitaka mamlaka husika kuangalia uwezekano wa kuweka utaratibu au sheria itakayowabana wakandarasi kuhakikisha wanawalipa wafanyakazi wao stahiki kwa wakati.

Waziri Mkuu Mwigulu alitoa agizo hilo kufuatia kuwepo malalamiko kwa baadhi ya wakandarasi, kutowalipa wafanyakazi wao katika miradi ya ujenzi.

Alitoa agizo hilo baada ya wananchi waliofanya kazi katika miradi mbalimbali, kueleza kero ya kutolipwa japokuwa wakandarasi hao tayari serikali imewalipa.

WABUNGE MKOANI RUKWA

Baadhi ya wabunge wa mkoa wa Rukwa waliipongeza serikali inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao ikiwemo ya afya, elimu na kilimo.

Mbunge wa Nkasi Kaskazini Salum Kazukamwe alisema ujenzi wa Hospitali ya Wilaya utarahisisha upatikanaji huduma bora za afya.

Previous Post

ATCL YARUDISHA WATANZANIA 236

Next Post

RAIS DK. SAMIA AIPAISHA TANZANIA MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI

Next Post
RAIS DK. SAMIA AIPAISHA TANZANIA MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI

RAIS DK. SAMIA AIPAISHA TANZANIA MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AWAPA KICHEKO KARAGWE

DK. SAMIA AWAPA KICHEKO KARAGWE

6 months ago
KOCHA MPYA ABEBESHWA MZIGO SIMBASC

KOCHA MPYA ABEBESHWA MZIGO SIMBASC

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?