• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

PALE PANAPOUMA ZAIDI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 18, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
PALE PANAPOUMA ZAIDI
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

NI dhahiri. Mashabiki wa Yanga wamejikuta katika maumivu ya hali ya juu baada ya timu yao kushindwa kuvuna pointi tatu katika mchezo wa pili mfululizo katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.

Yanga imeshindwa kuvuna pointi hizo dhidi ya TRA United katika mtanange uliomalizika kwa sare ya bila kufungana katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.

Kikosi cha Kocha Pedro Goncalves ambacho kilicheza mchezo huo bila ya nyota wake Ibrahim Hamad Bacca, Dickson Job, Depu na Chadrack Boka, haikuwa katika ubora wake uliozoeleka kutokana na wapinzani wao kuonyesha ushindani wa hali ya juu katika kuzuia.

Katika mtanange huo ulioanza saa 10:00 jioni, TRA United ya Kocha Ettiene Ndayoragije, ilikuwa katika kiwango bora hasa safu ya ulinzi na kiungo, ikizuia vyema na kuanzisha vizuri mashambulizi dhidi ya safu ya ulinzi ya Yanga iliyoundwa na Bakari Mwamnyeto, Asinki, Mohamed Hussein na Israel Mwenda.

Mechi hiyo iliyokuwa na kasi ya aina ya, timu zote zilishambuliana kwa zamu na mara nyingi mashambulizi yalikuwa yakitengenezwa pembeni.

Katika dakika ya 78, Mzamiru Yassin wa TRA United alitolewa nje kwa kadi mbili za njano baada ya kumchezea rafu Tshabalala.

Awali dakika ya 36, Mzamiru alipewa kadi ya kwanza ya njano kwa kumchezea rafu Shekhan Rashid.

Licha ya kuwa pungufu, timu hiyo iliendelea kukaba kwa nidhamu na kutengeneza nafasi za kushambulia, lakini ilikosa umakini wa kufunga.

Baada ya suluhu hiyo, Yanga inaendelea kuongoza ligi ikiwa na pointi 37, baada ya michezo 15, huku TRA United ikishika nafasi ya 10 na kujizolea pointi 20 baada ya kushuka dimbani mara 15.

Kabla ya sare ya jana, Yanga ilitoka suluhu dhidi ya Azam FC katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

TRA United: Jean Noel, Nasry Kombo, Valentin Nouma, Amy Mapaka, Karaboue Chamaou, Ramadhan Ramadhan, John Lazarus, Chande Chewe, Mzamiru Yassin, Jamali Dulaz na Joseph Akandwanaho.

Yanga: Djigue Diarra, Frank Assink, Bakari Mwanyeto, Maxi Nzengeli, Mohamed Damaro,

Previous Post

GAMONDI AITA JESHI LA MAANGAMIZI, MANULA NDANI

Next Post

WARIZI SANGU AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA NJOMBE MTAKA

Next Post
WARIZI SANGU AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA NJOMBE MTAKA

WARIZI SANGU AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA NJOMBE MTAKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

9 months ago
TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA

TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA

6 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?