• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MAKONDA : TUMEJIPANGA KUTWAA AFCON 2027

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 24, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
MAKONDA : TUMEJIPANGA KUTWAA AFCON 2027
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

AMINA KASHEBA Na NASRA KITANA

WAZIRI  wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Tanzania imejipanga kikamilifu kutwaa ubingwa wa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).

Akizungumza katika ufunguzi wa Kongamano la Idhaa za Kiswahili iliyofanyika jijini Arusha, Makonda amesema Tanzania kwa kushirikiana na Kenya na Uganda ina kila sababu ya kuwa na matumaini makubwa  ya kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Amesema  kipindi cha mashindano hayo itakuwa dirisha muhimu la kuitangaza Tanzania Bara na Zanzibar huku  matumizi ya lugha ya Kiswahili katika matangazo na mawasiliano ya mashindano hayo yatasaidia kukuza hadhi na ushawishi wa Kiswahili ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu.

“Mwakani mashindano ya AFCON, Zanzibar wamejipanga kikamilifu, Dar es Salaam wamejipanga na Arusha hivyo hivyo, miji yetu hii mikubwa mitatu ni ndoto yetu ichukue asilimia 60 ya mashindano ya Afcon 2027.

“Mashindano haya yanakwenda kuitangaza nchi yetu kufanya alama ya amani, mshikamano na utulivu, pia kuonyesha fursa za uchumi wa Tanzania, ” alisema Makonda.

Waziri huyo amesema  kuwa ushiriki wa Tanzania katika michuano hiyo unatoa nafasi ya kipekee ya kulitangaza taifa kimataifa.

KOCHA GAMONDI

Kocha wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’, Miguel Gamondi, amesema kikosi chake kipo fiti kuhakikisha kinapata ushindi katika mechi mbili za kirafiki za mashindano ya FIFA Series 2026.

Taifa Stars ambayo jana ilikwenda Rwanda kushiriki michuano hiyo, itavaana na Liechtenstein na kama itaibuka na ushindi itacheza na bingwa kati ya Aruba na Macau.

Akizungumza kabla ya kuondoka nchini, Gamondi amekiri mechi hizo zitakuwa ngumu lakini hana wasiwasi na kikosi chake kwani anaamini kitafanya vyema.

Gamondi raia wa Argentina, alisema kila mchezaji wake anafahamu umuhimu wa mechi hizo hivyo watahakikisha wanaonyesha kiwango bora kupata ushindi.

“Tumejipanga vizuri kwa mashindano hayo muhimu, lengo letu ni kuhakikisha tunashinda katika kila mchezo ili tufanye vizuri na kurejea nyumbani na ushindi,”  alisema Gamondi.

Naye beki wa timu hiyo, Bakari Mwanyeto alisema kila mchezaji yupo tayari kuipambaniua bendera ya Tanzania na anaamini michuano hiyo itawapa uzoefu mkubwa kwa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani.

“Tunakwenda katika mashindano haya tukiwa tumejiandaa vizuri kuhakikisha tunapambana ili kuonyesha uwezo tuliokuwa nao, pia yatatusaidia katika maandalizi ya AFCON,” alisema.

Kiungo Novatus Dismas, alisema: “Kila mchezaji yupo vizuri kwa michezo  ya FIFA Series, pia mwalimu ametuandaa vyema kiakili tufanye vizuri zaidi,”.

Naye kipa wa timu hiyo, Aishi Manula alisema amefurahi kurejea tena katika timu ya taifa na aliwakahikikishia Watanzania kuonyesha kiwango bora.

Previous Post

MGODI WA KIHISTORIA WA NIOBIUM KUJENGWA MKOANI MBEYA

Next Post

DK. KIKWETE ATEULIWA KUWA MWAKILISHI WA NGAZI YA JUU WA MWENYEKITI WA KAMISHENI YA AU

Next Post
DK. KIKWETE ATEULIWA KUWA MWAKILISHI WA NGAZI YA JUU WA MWENYEKITI WA KAMISHENI YA AU

DK. KIKWETE ATEULIWA KUWA MWAKILISHI WA NGAZI YA JUU WA MWENYEKITI WA KAMISHENI YA AU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIWANGO SIMBA CHAMKERA BARKER

KIWANGO SIMBA CHAMKERA BARKER

3 months ago
KIHONGOSI AWAPA SALAMU WATAKAOHUJUMU MIRADI

KIHONGOSI AWAPA SALAMU WATAKAOHUJUMU MIRADI

2 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?