• ePaper
Sunday, April 5, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home AFYA

DK. MWIGULU AELEZA MCHANGO WA SEKTA YA AFYA KATIKA UKUAJI UCHUMI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 1, 2026
in AFYA, Habari, Makala
0
DK. MWIGULU AELEZA MCHANGO WA SEKTA YA AFYA KATIKA UKUAJI UCHUMI
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

SEKTA ya afya ni mhimili mkuu wa maendeleo ya taifa lolote, hakuna uchumi imara bila jamii yenye afya bora na hakuna nguvu kazi yenye tija bila ustawi wa kimwili na kiakili wa wananchi.

Katika kuthibitisha hilo, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, imeweka mkazo mkubwa katika kuimarisha huduma za afya nchini, ikiongozwa na dhana kwamba afya ni mtaji wa maendeleo.

Tangu alipoingia madarakani, serikali yake imechukua hatua za kimkakati na haraka, kuboresha miundombinu ya afya, upatikanaji wa huduma, vifaatiba na dawa.

Hatua hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya kujenga taifa lenye wananchi wenye afya njema, linaloshiriki kikamilifu shughuli za uzalishaji mali na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa.

Moja ya mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi hiki, ni ujenzi wa hospitali 119 katika wilaya zote ambazo awali hazikuwa na hospitali za wilaya. Hatua hiyo imepunguza kwa kiasi kikubwa umbali ambao wananchi walilazimika kusafiri kufuata huduma za afya, na hivyo kuongeza upatikanaji wa huduma hizo kwa wakati na ufanisi zaidi.

Aidha, serikali imejenga vituo vya afya 649 na zaidi ya zahanati 2,700 kote nchini ambapo uwekezaji huo mkubwa katika ngazi za msingi za utoaji huduma, umeleta mageuzi makubwa katika mfumo wa afya, hasa maeneo ya vijijini, ambako changamoto ya upatikanaji huduma ilikuwa kubwa zaidi.

Kupitia juhudi hizo, wananchi wengi wanapata huduma karibu na maeneo yao, jambo linalopunguza vifo vinavyoweza kuzuilika na kuboresha ustawi wa jamii.

Katika kuimarisha zaidi sekta hiyo, serikali pia imeongeza uwekezaji katika ununuzi wa dawa na vifaatiba.

Pia, upatikanaji wa dawa muhimu umeboreshwa kwa kiwango kikubwa, huku juhudi zikifanyika kuhakikisha hospitali, vituo vya afya na zahanati zinakuwa na vifaa vya kisasa vinavyokidhi mahitaji ya sasa ya kitabibu.

Hatua hiyo imechangia kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa na kuimarisha imani ya wananchi kwa mfumo wa afya wa umma.

Vilevile, kukamilika ujenzi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa ya Katavi, Njombe, Songwe, Simiyu, Geita, Ruvuma, Shinyanga, Singida, Mara na Lindi ambazo zinatoa huduma mbalimbali zikiwemo huduma za dharura, mahututi, mama na mtoto, upasuaji magonjwa ya ndani, wagonjwa wa huduma za nje (OPD) na huduma za kusafisha figo ziwezesha wananchi kupata huduma karibu na maeneo wanayoishi.

Vilevile, alisema Rais Dk. Samia ameboresha sekta ya tiba nchini kwa kuimarisha mfumo wa BIMA ya Afya kwa Wote kwa wazee, watoto na wajawazito kwa utaratibu wa majaribio.

Aidha, katika kuendelea kuboresha huduma za afya, serikali imeongeza upatikanaji wa vifaatiba ikiwemo MRI kutoka 7 hadi 13, CT Scan 13 hadi 45, Mini Angio Suite 4 hadi 5, Fluoroscopy 9 hadi 13, Digital X-Ray 147 hadi 559, Ultrasound 476 hadi 970 na Oxygen Plant 25.

Hata hivyo, wakati serikali inaendelea kuongeza uwekezaji katika sekta mbalimbali ikiwemo ya afya ili kuboresha huduma kwa wananchi, hali halisi inayojitokeza katika baadhi ya maeneo inaibua maswali kuhusu uwajibikaji wa watendaji na ufanisi wa usimamizi wa rasilimali za umma.

Mbali na serikali kuendelea kuongeza bajeti katika sekta ya afya kwa lengo la kuboresha huduma, ikiwa ni pamoja na ununuzi wa dawa, vifaatiba na vitendanishi baadhi ya wananchi wanashindwa kupata huduma wanazostahili wanapokwenda katika vituo vya kutolea huduma hizo.

Akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Katavi hivi karibuni, Dk. Mwigulu alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kupitia mikutano ya hadhara, ambapo wengi wao walidai kukosa dawa wanapokwenda katika vituo vya kutolea huduma hizo.

Kufuatia malalamiko hayo, Waziri Mkuu alimwagiza Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi, Sipha Mwanjala, kufanya uchunguzi wa kina kubaini kama kuna uzembe, mianya ya ubadhirifu au udhaifu katika mfumo wa usambazaji wa dawa.

Ripoti zinaonesha upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya zikiwemo hospitali ni zaidi ya asilimia 90.

Hali hiyo inasababisha mkanganyiko kati ya takwimu za kiutendaji na hali halisi iliyopo vituoni, hivyo Waziri Mkuu alihoji inakuwaje duka la mtu binafsi linakuwa na dawa wakati serikali inakosa? “Huo ni mchezo ambao haukubaliki. Uchunguzi ufanyike kubaini mtiririko wa dawa na fedha zake. Takwimu nzuri katika ripoti za kiutendaji hazina maana iwapo wananchi hawapati huduma wanazostahili,” alisema.

Hata hivyo, uhalisia unaosimuliwa na wananchi pamoja na hali inayoonekana katika hospitali nyingi ni tofauti na takwimu hizo. Wagonjwa wengi wanapofika hospitalini hupatiwa maelekezo ya kwenda kununua dawa katika maduka ya watu binafsi, jambo linaloongeza gharama kwa wananchi na kupunguza imani yao kwa huduma za afya za umma.

Waziri Mkuu alisisitiza watendaji wanapaswa kutambua dhamira ya serikali ni kuwahudumia wananchi, hivyo ni wajibu wao kuhakikisha fedha zinazotolewa kwa ajili ya huduma muhimu kama za afya zinatumika kwa uadilifu na ufanisi na kwamba hakuna atakayevumiliwa kwa kukiuka maadili.

Waziri Mkuu alisema serikali haiwezi kuvumilia kuona wananchi wengi bado wanalazimika kununua dawa katika maduka ya watu binafsi wanapokwenda kutibiwa hospitalini, huku serikali ikitumia fedha nyingi kugharimia ununuzi wa dawa na vifaatiba kwa ajili ya wananchi.

Aidha, kutokana na umuhimu wa sekta ya afya, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuzingatia Sera za Chama cha Mapinduzi (CCM), amesimamia serikali kuimarisha afya za wananchi ili washiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kuchangia kuongezeka kwa kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa.

Kwa kutambua juhudi hizo kubwa za Rais Dk. Samia, Waziri Mkuu aliendelea kusisitiza watumishi katika sekta ya afya kuwa waadilifu na waaminifu katika kusimamia matumizi bora ya dawa na vifaatiba katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini.

Alisema Rais Dk. Samia, amesimamia kuendelea kwa Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kutolea huduma za afya, kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kutoa huduma, kuongeza dawa, vifaa, vifaatiba na vitendanishi katika vituo vya kutolea huduma za afya na kuimarisha huduma za ubingwa na ubingwa bobezi.

Waziri Mkuu alisema Rais Dk. Samia ameondoa gharama za matibabu ya vipimo vya kibingwa kwa magonjwa sugu yasiyoambukiza kama saratani, figo, moyo, sukari, mifupa na mishipa ya fahamu, pia amepiga marufuku hospitali kuzuia miili ya marehemu kuchukuliwa kwa sababu ya deni la gharama za matibabu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko, alisema hadi kufikia Februari, mwaka huu, sekta ya afya imepoke sh. bilioni 43.962 kuboresha huduma za afya, ununuzi wa vifaa na vifaatiba, ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Pia, Mrindoko aliongeza kuwa fedha hizo zimetumika katika ujenzi wa hospitali nne za wilaya, ujenzi wa vituo vya afya 11, ujenzi wa zahanati 50 na ukarabati wa Hospitali Kongwe ya Manispaa ya Mpanda  na ukarabati wa vituo vya afya na Zahanati.

Aidha, alisema kumekuwa na ongezeko la vituo vya kutolea huduma za afya ambapo kwa mwaka 2020, mkoa ulikuwa na vituo 102 vya kutolea huduma za afya na hadi kufikia Februari, mwaka huu ulikuwa na vituo vya kutolea huduma za afya 168 ikiwa ni ongezeko la vituo 66 sawa na asilimia 64.7.

Alisema katika kuongeza ubora wa huduma za afya Mkoa wa Katavi, umeendelea kuomba vibali vya ajira kutoka serikali Kuu ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa ngazi ya Mkoa na halmashauri, ambapo hadi kufikia Januari, mwaka huu.

Mkoa ulikuwa na watumishi 1,914 kati ya watumishi 4,873 wanaohitajika. “Ikilinganishwa na mwaka 2020 ambapo mkoa ulikuwa na watumishi 654 hii ni sawa na ongezeko la watumishi 1,260.”

Mkuu huyo wa mkoa alisema katika kipindi cha Januari, 2026 mkoa ulipokea watumishi 311 wa kada mbalimbali za afya, ongezeko hilo linatokana na utekelezaji wa ahadi za siku 100 za Rais Dk. Samia ambapo watumishi hao watawezesha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi kwa urahisi na wakati.

Previous Post

SERIKALI KUENZI MEMA YA LUKUVI

Next Post

WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

Next Post
WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

WIZARA YA VIWANDA YAZALISHA AJIRA LUKUKI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WACHINA WANAODAIWA KUKUTWA NA MABILIONI WAPANDISHWA KORTINI

WACHINA WANAODAIWA KUKUTWA NA MABILIONI WAPANDISHWA KORTINI

3 months ago
SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

4 weeks ago

Popular News

  • CHAMUDATA YAZUNGUMZIA AMANI

    CHAMUDATA YAZUNGUMZIA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MCHENGERWA ASHUSHA MAAGIZO KWA WAGANGA WAKUU WA MIKOA, WILAYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AELEZA FAIDA YA KULINDA TUNU YA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UTEUZI WA PROFESA KABUDI GUMZO NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VIONGOZI WA DINI WAHUBIRI AMANI 

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?