• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 27, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mussa Yusuph,

Lindi

KIMBUNGA cha Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, kimeendelea kushika kasi kwa kusambaratisha ngome mbalimbali za vyama vya upinzani mkoani Lindi.

Hali hiyo imeendelea kudhihirika katika mikutano ya kampeni za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, ambapo vigogo kutoka vyama hivyo, waliamua kujiunga CCM, huku wakieleza kuguswa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na mazuri yaliyopo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2025–2030).

katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Ilulu mkoani Lindi, wanachama kutoka vyama vya CHADEMA, CHAUMMA na CUF wamerejesha kadi za vyama hivyo kisha kupokelewa CCM mbele ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Dk. Samia.

Akizungumza katika mkutano huo, aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Lindi na Makamu Mwenyekiti Kanda ya Kusini, Salum Bar’wan, alisema ameguswa na Ilani ya CCM 2025–2030, ikiwemo dhamira ya kuufungua Mkoa wa Lindi kupitia uboreshaji wa miundombinu ya barabara, ujenzi wa uwanja wa ndege na utekelezaji mradi wa kimkakati wa gesi asilia (LNG).

Alisema ameamua kujiunga CCM kwa sababu kimeonesha dira ya maendeleo ya kweli, huku akiwataka wananchi wa Lindi kujitokeza kwa wingi kumpa kura Dk. Samia.

Naye, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mchinga kupitia CHAUMMA, Yusuph Issa Tamba, alisema amefikia uamuzi huo kwa ridhaa yake mwenyewe bila kushawishiwa na mtu yeyote.

“Natuma salamu kwa chama changu wametuma ujumbe wa vitisho, waambieni mimi siyo mtoto mdogo, sitishiki. Huku ndiyo nyumbani, mitano tena. Nimerudi nyumbani, naomba mnipokee,” alisema.

Tamba aliahidi kushirikiana na CCM kuhakikisha ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 na kuwataka  wananchi wa Mchinga na Mkoa wa Lindi kwa ujumla kuunga mkono maendeleo yanayoletwa na Dk. Samia.

Previous Post

DK. SAMIA KULETA TEKNOLOJIA YA KILIMO

Next Post

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Next Post
MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAASKOFU WABEBA AJENDA YA UMOJA

MAASKOFU WABEBA AJENDA YA UMOJA

1 week ago
SERIKALI YATOA TAMKO

SERIKALI YATOA TAMKO

5 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?