• ePaper
Sunday, July 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 14, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

WAKATI Ligi Kuu Tanzania Bara ikisimama kupisha mechi za kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026, Simba ndiyo timu iliyofunga mabao mengi katika michuano hiyo hadi sasa msimu huu.

Katika michuano hiyo mikubwa zaidi kwa ngazi za klabu nchini, jumla ya mabao 36 yamefungwa msimu huu, huku Simba ikipachika mabao sita.

Kwa mujibu wa msimamo wa ligi hiyo, jumla ya michezo 20 imechezwa ambapo baadhi ya timu zimeingia dimbani mara mbili na nyingine mara tatu.

Katika mchanganuo wa mabao, Simba inafuatiwa na JKT Tanzania na Dodoma Jiji zilizofunga mabao manne kila moja.

Yanga na Azam FC zimepachika mabao matatu kila moja zikifuatiwa na Singida Black Stars, Mashujaa, Namungo, Mtibwa Sugar, Coastal Union na Tabora United zilizopachika mabao mawili.

Timu zilizofunga bao moja ni Mbeya City, Tanzania Prisons, KMC na Pamba Jiji.

Hata hivyo ni Fountain Gate pekee ambayo hadi sasa haijapachika bao lolote katika mitanange mitatu iliyocheza msimu huu.

Akizungumza kwa njia ya simu, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema kikosi chao kimedhamiria kufanya vyema zaidi msimu huu.

“Sisi ni timu kubwa na tunahitaji mambo makubwa, huu ni mwanzo tu na Wanasimba wanapaswa kujua kwamba tuna timu ya kutoka kifua mbele kufanya makubwa katika kila mechi,” alisema.

Previous Post

JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

Next Post

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

Next Post
DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TUME ILIYOUNDWA NA RAIS DK. SAMIA ILIVYOBEBA MATUMAINI YA AMANI

TUME ILIYOUNDWA NA RAIS DK. SAMIA ILIVYOBEBA MATUMAINI YA AMANI

3 months ago
DK. MWIGULU AWAVAA WANAOSUBIRI UTEUZI

DK. MWIGULU AWAVAA WANAOSUBIRI UTEUZI

5 months ago

Popular News

  • KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA AIPA JEURI YANGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWALIMU, GUEYE WAPO SIMBA SANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI ASHTUKIA ‘USANII’ WA WACHIMBAJI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?