• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

NJOONI MUONE SHOO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 22, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
NJOONI MUONE SHOO
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI leo ikishuka dimbani dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco, timu ya soka Yanga imesema ipo fiti kuhakikisha inapata ushindi katika mtanange huo wa kwanza wa kundi B wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Yanga itachuana na AS FAR saa 10:00 jioni katika mechi itakayopigwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Akizungumza kutoka Zanzibar, Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves, amesema hana presha na mchezo huo kwani wamejipanga kupata ushindi.

Pedro amesema pamoja ya kutofanya mazoezi ya kutosha na kikosi chake lakini ana imani watapata matokeo mazuri katika mchezo huo.

Kocha huyo amesema hana hofu na kikosi chake kwani anajua ubora wa wachezaji wake na jinsi wanavyojituma uwanjani.

 “Tunaingia katika mchezo mgumu, hatuna presha na wala hakuna ambaye tunamhofia, tuna matumaini makubwa ya kupata ushindi kutokana na mbinu pamoja mifumo ambayo nimewafundisha wachezaji wangu,” amesema Pedro.

Kocha huyo amesema wamefanya marekebisho mapungufu yote yaliyojitokeza katika mechi zilizopita ili kufanya vizuri katika mchezo huo.

Amesema lengo lao kubwa ni kuhakikisha timu yake inashinda katika mchezo huo na inayofuata ili kumaliza kundi ikiwa nafasi ya kwanza.

Naye nyota wa timu hiyo, Dikson Job amesema wachezaji wanajua umuhimu wa mchezo huo na wamejipanga kupambana kwa jasho na damu kupata ushindi.

“Huu ni mchezo muhimu kwetu kupata ushindi hasa katika uwanja wetu wa nyumbani, hatuna hofu na wachezaji wote tumejipanga vyema kuhakikisha hatupotezi na kujizolea pointi tatu muhimu,” amesema Job.

Katika mashindano hayo, Yanga ipo kundi B na timu za Al Ahly ya Misri, AS FAR ya Morocco na JS Kabyile ya Algeria.

Previous Post

DK. NCHIMBI ATAJA FAIDA UKARABATI RELI TAZARA

Next Post

SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA

Next Post
SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA

SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIHONGOSI AANIKA UIMARA WA CCM KWA WATANZANIA

KIHONGOSI AANIKA UIMARA WA CCM KWA WATANZANIA

2 months ago
WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?