• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Biashara

SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 22, 2025
in Biashara, Kimataifa, Michezo
0
SIMBASC YAITA MASHABIKI KWA MKAPA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI Simba ikitarajiwa kuvaana na Petro de Luanda kesho, uongozi wa Wekundu hao wa Msimbazi wamewaomba mashabiki wake kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kuisapoti miamba hiyo.

Simba itachuana na Petro de Luanda saa 10:00 jioni katika mchezo wa kwanza wa kundi D wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Akizungumza Dar es Salaam, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, alisema ni muhimu mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kuhakikisha miamba hiyo inashinda kuanza vyema katika kundi hilo.

Ahmed amesema ili kupata matokeo mazuri, mashabiki wao wanatakiwa kuonyesha sapoti kubwa katika mchezo huo.

Amesema huo ni mchezo mgumu kwao kulingana na hatua ambayo wapo kwani hivi sasa kila timu inatafuta pointi tatu, hivyo wanapaswa kutumia vyema uwanja wa nyumbani kupata matokeo mazuri.

 “Huu ni mchezo muhimu kwetu kwani tunahitaji kupata ushindi katika mchezo huu mgumu, hivyo mashabiki wanatakiwa kujaa kwa wingi kuwapa nguvu wachezaji wetu hasa tukiwa katika uwanja wetu wa Mkapa, mchezo wetu wenyewe na mashabiki wanajua furaha ipo katika ushindi hilo ni jukumu la wachezaji kutupambania mpaka mwisho,” amesema Ahmed.

Amesema lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanapata ushindi katika kila mchezo wa nyumbani na ugenini hivyo ni muhimu mashabiki kuwapa sapoti ya kutosha wachezaji wao ili kufanikisha.

Meneja huyo amesema hawana hofu na kikosi walichokuwa nacho kwani kila mmoja anajua umuhimu wa mchezo huo na wengi wao ni wazoefu katika mashindano hayo.

Katika hatua hiyo Simba imepangwa kundi D ikiwa na timu za timu za Esperance Sportive kutoka Tunisia, Petro De Luanda ya Angola na Stade Malien kutoka Mali.

Previous Post

NJOONI MUONE SHOO

Next Post

AMANI NGUZO KUU YA USTAWI – RAIS DK. SAMIA

Next Post
AMANI NGUZO KUU YA USTAWI – RAIS DK. SAMIA

AMANI NGUZO KUU YA USTAWI – RAIS DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WADAU WAFICHUA AMANI INAVYOVUTIA WAWEKEZAJI

WADAU WAFICHUA AMANI INAVYOVUTIA WAWEKEZAJI

2 weeks ago

GAMONDI AJA KIVINGINE KUIVAA MOROCCO AFCON

3 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?