• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA YAPEWA MCHONGO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 26, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
SIMBA YAPEWA MCHONGO
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

UONGOZI wa Simba umetakiwa kuboresha safu ya ushambuliaji kuhakikisha inapata matokeo mazuri mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Keshokutwa, Simba itashuka dimbani ikiwa ugenini kupambana na Stade Malien ya Mali katika mchezo wa pili wa CAFCL hatua ya makundi.

Simba itaingia katika mchezo huo, ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza bao 1-0 mbele ya Atletico Petro de Luanda, nyumbani, mechi ya kwanza hatua ya makundi iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam huku Stade Malien ikilazimishwa suluhu ugenini dhidi ya Esperance Sportivo de Tunis ya Tunisia.

Simba ilianza michuano hiyo hatua ya awali msimu huu kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Gaborone United kabla ya sare ya 1-1 nyumbani, baadaye ilishinda mabao 3-0 dhidi ya Nzingizi Hotspur kabla ya suluhu ya nyumbani.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa  katika hatua ya awali ya kufuzu kucheza makundi ya CAFCL, Stade Malien ilishinda 5-0 dhidi ya Tempele Macaf kabla ya kuichakaza 2-0 ikiwa nyumbani.

Mechi za hatua ya kwanza, Malien ilitoka sare ya 1-1 dhidi ya Noudhibou mchezo wa marudiano ikishinda mabao 2-0.

Katika mechi ya kwanza hatua ya makundi, ikiwa ugenini Stade Malien ililazimishwa suluhu dhidi ya Esperance Sportivo de Tunis ya Tunisia.

Timu hiyo itaikaribisha Simba katika mchezo wa pili wa hatua ya makundi utakaofanyika keshokutwa nchini Tunisia.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, wadau wa soka walisema Simba inatakiwa kufanya uboreshaji wa safu ya ushambuliaji kuhakikisha inafanya vyema kimataifa.

Kocha na mchezaji wa zamani wa Yanga, Charles Mkwasa alisema uongozi wa Simba unatakiwa kuboresha eneo la ushambuliaji kuhakikisha timu inafanya vizuri katika mechi zitakazofuata.

Alisema Simba haikuwa na sababu ya msingi kupoteza mechi ya kwanza kwani walikuwa nyumbani na walitengeneza nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia vizuri.

Alisisitiza wachezaji wa Simba walikuwa wakipoteza mipira katika maeneo muhimu kitu.

“Simba walicheza mechi,  lakini haikuwa sahihi wao kufungwa kutokana na umakini mdogo ndiyo maana walipoteza.

“Kiufundi walionekana wana udhaifu safu ya ushambuliaji ikiwemo kupoteza mipira katika sehemu muhimu kitu kilichowapa ugumu kupata ushindi huku wapinzani wakiwa na kasi hasa ya kushambulia.

“Uongozi unatakiwa kufanyia kazi kasoro hizo, hasa katika eneo la ushambuliaji, bado  wana mechi nyingi kama wakibadilika wanaweza kufika mbali zaidi,” alisema.

Mchezaji wa zamani wa Simba, Yanga na Taifa Stars, Zamoyoni Mogella alisema uongozi wa Simba unatakiwa kufanyia kazi upungufu uliyojitokeza katika mchezo wa kwanza hasa safu ya ushambuliaji.

Alisema Simba ilitengeneza nafasi nyingi lakini ilishindwa kuzitumia kutokana na washambuliaji wake kutokuwa makini kukwamisha mipira wavuni.

Alisema safu ya ushambuliaji inatakiwa kufanyiwa kazi kuhakikisha wanawajibika kufunga mabao mengi.

“Simba haikucheza katika kiwango ambacho wengi tulikitarajia tangu awali kutokana na makosa mbalimbali waliyoyafanya.

“Safu ya ushambuliaji inatakiwa kufanyiwakazi kuhakikisha timu inatumia nafasi nyingi wanazozitengeza na kupachika mabao,” alisema Mogella.

Wakati huo huo, uongozi wa timu hiyo umeweka wazi kuwa bado haujakata  tamaa kwani wanajipanga kwa ajili ya mchezo unaofuata utakaopigwa Novemba 30, mwaka huu wakiwa ugenini.

Pambano hilo limepangwa kufanyika Stade Malien ya Mali mchezo utakaochezwa Uwanja wa 26 Mars.

Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema kuwa pamoja na kupoteza mchezo wa kwanza lakini bado hawajakata tamaa.

 “Tumepoteza mchezo mmoja tu, ndio imetuumiza kwa kiasi kikubwa lakini hatujakata tamaa, tutapambana kuhakikisha tunashinda katika mechi zilizobakia za kundi letu,” alisema Ahmed.

Hata hivyo, Ahmed alisema kuwa timu yao inatarajiwa kuondoka jijini, Novemba 27 mwaka huu kwenda Mali kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo wao dhidi ya Stade Malien.

Alisema kuwa mwalimu ametaka timu yao isafiri mapema ili kwenda kurekebisha mapungufu yaliojitokeza katika mchezo wa kwanza.

Hadi sasa, Simba inaburuza mkia katika Kundi D linaloongozwa na Petro de Luanda, huku nafasi ya pili ikishikiliwa na Espérance Sportive de Tunis yenye pointi moja, sawa na Stade Malien ya Mali.

Simba ipo kundi D ikiwa na timu za timu za Esperance Sportive kutoka Tunisia, Petro De Luanda ya Angola na Stade Malien kutoka Mali.

Previous Post

YANGA, JS KABYLIE  NAMBA ZINAONGEA

Next Post

TUTAILINDA NCHI YETU KWA GHARAMA – PM MWIGULU

Next Post
TUTAILINDA NCHI YETU KWA GHARAMA – PM MWIGULU

TUTAILINDA NCHI YETU KWA GHARAMA – PM MWIGULU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASOMI, WACHAMBUZI WATOA NENO SERIKALI KUWEZESHA VIJANA

WASOMI, WACHAMBUZI WATOA NENO SERIKALI KUWEZESHA VIJANA

4 months ago
MWANASHERIA WA KWANZA MWANAMKE UDSM AFARIKI

MWANASHERIA WA KWANZA MWANAMKE UDSM AFARIKI

4 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?