• ePaper
Saturday, May 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WAZIRI CHONGOLO AELEKEZA MIFUMO TOSCI ISOMANE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 27, 2025
in Habari, Kitaifa
0
WAZIRI CHONGOLO AELEKEZA MIFUMO TOSCI ISOMANE
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HAPPINESS MTWEVE, Dodoma

WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, ameitaka Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), kuhakikisha sheria inazozisimamia, zinasomana na taasisi nyingine kuimarisha utendaji kazi.

Taasisi hizo ambazo zimeagizwa mifumo yake isomane na TOSCI ni pamoja na Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI).

Alisema utekelezaji wa majukumu yao ni shirikishi, hiyo itaongeza wigo wa uzalishaji mbegu kwa kushirikiana na sekta binafsi.

Chongolo alisema hayo jijini hapa, alipokutana na viongozi mbalimbali, wakiwemo Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI),

Alisema katika kutekeleza malengo na mikakati iliyopangwa na Wizara na Taasisi zake, viongozi wana wajibu wa kuhakikisha kazi hizo, zinakuwa na manufaa kwa wakulima.

“TOSCI ninawaelekeza, sheria mnazosimamia kama mamlaka zinasomana na Taasisi za TARI na ASA kwa kuwa utekelezaji wake unashabihiana,”alisema.

Aidha, aliitaka ASA kuongeza wigo wa uzalishaji mbegu kwa kushirikiana na sekta binafsi, huku akiitaka TARI kuongeza utafiti zaidi katika zao kama kokoa.

Pia, Chongolo aliiagiza TARI kuwafikiria watafiti wa mbegu ili wanufaike na utafiti wao, kama kuongeza umri wa kustaafu kwa watafiti wabobezi.

Akizumgumzia miradi inayoendelea chini ya wizara hiyo na taasisi zake, Chongolo alitaka ikamilishwe kwa wakati kwa mujibu wa mikataba.

Previous Post

SIMBACHAWENE AHIMIZA KUDUMISHA ZAIDI AMANI

Next Post

RAIS DK. SAMIA APONGEZWA UAMUZI SHEREHE ZA UHURU

Next Post
RAIS DK. SAMIA APONGEZWA UAMUZI SHEREHE ZA UHURU

RAIS DK. SAMIA APONGEZWA UAMUZI SHEREHE ZA UHURU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TUSHEREHEKEE EID KWA UTULIVU, AMANI

TUSHEREHEKEE EID KWA UTULIVU, AMANI

2 months ago
MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

3 weeks ago

Popular News

  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?