RABAT, Morocco
KOCHA wa timu ya taifa ya Gabon, Thierry Mouyouma, amesema mipango yake ni kufika nusu fainali katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON 2025).
Kocha Mouyouma alisisitiza amejipanga kufanya vyema katika michuano hiyo na mipango yake ni kufika hatua ya nusu fainali.
Alisema kikosi chake kimesheheni wachezaji wenye uwezo mzuri wa kumsaidia kufanya vyema katika michuano hiyo msimu huu.
Alisema alishapata uzoefu wa michuano hiyo akiwa kama mchezaji, hivyo ana imani atatumia mbinu mbalimbali kuhakikisha anafikia malengo msimu huu.
“Nitatumia uozefu wangu katika michuano ya AFCON 2025 kuhakikisha tunafikia malengo tuliyojiwekea.
“Nilipata uzoefu nikiwa mchezaji, hivi sasa ni kocha, hivyo ninaamini tutafanya vizuri katika michuano ya msimu huu na kufika hatua ya nusu fainali,” alisema.
Alisema anatambua wamepangwa kundi lenye timu zenye uzoefu na michuano hiyo, lakini wamejipanga kupambana ili kutimiza malengo waliyojiwekea.
(BBC)




