• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MASHINA NI MOYO WA CCM – DK. ASHA-ROSE MIGIRO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 13, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MASHINA NI MOYO WA CCM – DK. ASHA-ROSE MIGIRO

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Asha-Rose Migiro

0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Asha-Rose Migiro, amesema uimara wa CCM unatokana na wanachama wake kujitokeza kikamilifu katika mikutano ya chama kwa kuwashirikisha wanachama wa CCM pamoja na wananchi wasiokuwa wanachama, hali inayokifanya chama hicho kuendelea kuwa imara na chenye mvuto kwa Watanzania.

Akizungumza na mabalozi wa mashina na wanachama wa CCM katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam, Dk. Migiro amesema ubora wa CCM unatokana na siasa zake za kujenga hoja na kuimarisha imani ya kudumu kwa wananchi, akisisitiza kuwa misingi hiyo imeifanya CCM kuwa chama chenye uthabiti wa kisiasa kwa miaka mingi.

Ameeleza kuwa chama kimeweka utaratibu madhubuti wa kuimarisha vikao vya mashina kwa kukutana mara kwa mara, akibainisha kuwa mikutano hiyo ni nyenzo muhimu ya kusikiliza wananchi, kujenga mshikamano na kuimarisha demokrasia ya ndani ya chama.

Dk. Migiro amesisitiza kuwa itikadi ya CCM itaendelea kujengwa juu ya misingi ya utu, ujamaa na kujitegemea kama inavyobainishwa kwenye kauli mbiu ya chama “Kazi na Utu, Tunasonga Mbele”, akieleza kuwa dhamira ya CCM ya kushika Dola inalenga kujenga utu wa Mtanzania kwa kuboresha maisha yao kupitia ujenzi wa miundombinu, hospitali na huduma nyingine za kijamii.

Akifafanua nafasi ya mashina ndani ya chama, alisema licha ya kuonekana kama ngazi ndogo ya uongozi, mashina ndiyo nguzo kuu inayobeba uimara na umadhubuti wa CCM. “Mashina ni moyo wa Chama Cha Mapinduzi,” amesisitiza.

Aidha, ametoa wito kwa wanachama kushiriki kikamilifu katika vikao vya mashina na kuendelea kutangaza maendeleo yanayopatikana chini ya uongozi wa CCM, huku akiwataka mabalozi kuenzi alama za chama, kuendesha mikutano kwa nidhamu na kuwashirikisha wananchi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AHIMIZA AMANI, MSHIKAMANO

Next Post

JASHO LIMEMWAGIKA

Next Post
JASHO LIMEMWAGIKA

JASHO LIMEMWAGIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

AELEZA CCM ITAKAVYO JENGA UCHUMI JUMUISHI

AELEZA CCM ITAKAVYO JENGA UCHUMI JUMUISHI

8 months ago
BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO DODOMA

BUNGE LA 13 KUANZA RASMI KESHO DODOMA

6 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?