• ePaper
Friday, April 24, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

JASHO LIMEMWAGIKA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 14, 2026
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
JASHO LIMEMWAGIKA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

JASHO limemwagika. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya Yanga na Azam FC jana, kuonyesha moja kati ya fainali bora katika historia ya Kombe la Mapinduzi.

Katika fainali hiyo iliyopigwa Uwanja wa Gombani, Pemba, Yanga ilitwaa ubingwa kwa mikwaju ya penalti 5-4 kufuatia timu zote kumwaga jasho kwa zaidi ya dakika 120 bila ya kufungana.

Wakati kipa wa Azam FC, Aishi Manula, akionyesha umahiri mkubwa katika dakika 120, kipa wa Yanga, Abubakar Mshery aligeuka shujaa wa timu yake baada ya kuokoa mkwaju wa penalti ulioipa ushindi miamba hiyo.

Wachezaji wa Yanga waliofunga penalti ni Emmanuel Mwanengo, Prince Dube, Pacome Zouzoua, Mudathir Yahya na Bakari Mwamnyeto.

Wakati mkwaju wa penalti wa Landry Zouzou ukidakwa na Mshery, nyota wa Azam FC walioweka kimiani mikwaju hiyo ni Yahya Zayd, Sadio Kanoute, Twalibu Nuru na Kamanya.

Katika dakika 90, timu zote zilishambuliana kwa zamu huku makipa wa timu zote wakionyesha umahiri wa kuzuia michomo mbalimbali.

Hata hivyo, dakika ya 72, nyota wa Azam FC, Cheickna Diakite  alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano.

Licha ya kuwa pungufu, Azam FC iliendelea kuwa na utulivu katika eneo la ulinzi hatua ambayo iliifanya Yanga kuwa na wakati mgumu wa kupata bao.

Baada ya dakika 90 kumalizika, timu hizo ziliongezewa dakika 30, ambapo katika dakika ya 114, Yanga ilipata penalti baada ya beki wa Azam FC, Twalibu Nuru, kuushika mpira ndani ya eneo la hatari katika harakati za kutaka kuokoa mpira.

Hata hivyo, kipa Aishi Manula aliendelea kuibakisha Azam FC mchezoni baada ya kuokoa penalti hiyo iliyopigwa na staa Pacome Zouzoua dakika ya 115.

Azam FC: Aisha Manula, Nathaniel Chilambo, Landry Zouzou, Lameck Lawi, Twalib Nuru, Himid Mao/ Sadio Kanoute, Zidane Sereri, Feisal Athuman, Jephet Kitambala/ Yoro Diaby , James Akaminko/ Yahya Zayd na Cheickna Diakite.

Yanga: Abuutwalib  Mshery, Kibwana Shomary/ Bakari Mwanyeto,  Chadrack Boka/Mohamed Hussein. Dickson Job, Ibrahim Bacca, Moussa Bala Conte, Maxi Nzengeli/ Sheikhan Abdallah, Duke Abuya/ Mudathir Yahya, Prince Dube, Pacome Zouzou na Celestin Ecua/Edmund John/ Emmanuel Mwanengo.

Previous Post

MASHINA NI MOYO WA CCM – DK. ASHA-ROSE MIGIRO

Next Post

NUSU FAINALI YA VIGOGO AFCON

Next Post
NUSU FAINALI YA VIGOGO AFCON

NUSU FAINALI YA VIGOGO AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

HISTORIA YA HESHIMA

HISTORIA YA HESHIMA

2 months ago
SIMBA SC YAWATOA HOFU MASHABIKI KUHUSU BAJABER

SIMBA SC YAWATOA HOFU MASHABIKI KUHUSU BAJABER

5 months ago

Popular News

  • 4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AWASHUKIA WACHOCHEZI MIGOGORO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UKWELI HADHARANI TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YASIJIRUDIE TENA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?