• ePaper
Friday, April 24, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

ROONEY KUREJEA MAN UNITED

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 14, 2026
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
ROONEY KUREJEA MAN UNITED
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

MANCHESTER, England

MKONGWE Wayne Rooney, amesema yupo tayari kurejea kuongeza nguvu katika benchi la ufundi la klabu hiyo kama Michael Carrick atafanikiwa kuteuliwa kuwa kocha wa kikosi hicho.

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya England, alishacheza pamoja na Rooney ambapo yupo katika rada za kukabidhiwa timu hadi mwishoni mwa msimu huu.

Uongozi wa Manchester United ulimfuta kazi hivi karibuni aliyekuwa kocha Ruben Amorim kutokana na mwenendo mbovu wa matokeo msimu huu.

Hivi sasa uongozi wa klabu hiyo unahaha kutafuta kocha mpya kwa ajili ya kuendelea alipoishia Amorim hadi mwishoni mwa msimu huu.

Vilevile, kiungo wa zamani raia wa Scotland, Darren Fletcher, aliyewahi kucheza pamoja na Rooney ndani ya United, hivi sasa amepewa timu kwa muda.

Taarifa kutoka katika mtandao wa klabu, zinasema huenda Carrick akaanza kukonoa kikosi hicho kitakaporejea mazoezini leo.

Rooney alisema kuwa yupo tayari kushirikiana na Carrick kama atatangazwa kuwa kocha wa kikosi hicho.

Alisema Carrick ni mmoja wa watu wanaofaa kuingoza United kwani alishacheza muda mrefu na kuipatia mafanikio makubwa.

Alisema hivi sasa wanatakiwa watu wanaoijua timu hiyo kiundani kuhakikisha wanaiongoza na kurejesha matumaini yaliyopotea kwa mashabiki na wadau wa United.

“Carrick ndiye mtu anayeweza kurejesha matumaini ndani ya kikosi cha Manchester United hivi sasa, nipo tayari kushirikiana naye kuhakikisha timu inarejea katika ubora wake.

“Wanaotakiwa kuiongoza United hivi sasa ni watu kama Darren Fletcher, John O’Shea, Carrick au mimi ambao tunaitambua timu kwa kiasi kikubwa na kuhakikisha inarejesha makali yake katika msimu huu.

“Timu imeshapoteza imani kwa mashabiki inatakiwa kufanyika kazi ya ziada kuhakikisha inarejesha matumaini kwa mashabiki na familia za mpira,” alisema.

Katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, hivi sasa Manchester United ipo nafasi ya saba ikiwa na pointi 32 baada ya kucheza mechi 21 msimu huu.

(BBC)

Previous Post

NUSU FAINALI YA VIGOGO AFCON

Next Post

DRC WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUTOA HIFADHI YA WAKIMBIZI

Next Post
DRC WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUTOA HIFADHI YA WAKIMBIZI

DRC WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUTOA HIFADHI YA WAKIMBIZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SARE ZA SHULE ZISIWE KIKWAZO – MARC

SARE ZA SHULE ZISIWE KIKWAZO – MARC

4 months ago
BARKER ALIA NA NAFASI SIMBA

BARKER ALIA NA NAFASI SIMBA

3 months ago

Popular News

  • 4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    4 ZAONGOZA KWA UKAME WA MABAO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AWASHUKIA WACHOCHEZI MIGOGORO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UKWELI HADHARANI TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YASIJIRUDIE TENA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MSD YABAINISHA DHAMIRA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA YA AFYA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?