• ePaper
Sunday, September 13, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 11, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto mchanga wa kike leo tarehe 11 Machi, 2026, katika makazi yake, Ikulu Chamwino, jijini Dodoma.

Mtoto huyo aliyepewa jina la Grace Samia Suluhu, alitelekezwa mjini Nzega, mkoani Tabora, amekabidhiwa kwa Rais Dk. Samia.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mtoto huyo, Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitapwaki Tukai, amesema mtoto huyo aliokotwa  Januari 17, 2026 akiwa ametelekezwa katika jirani na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega mjini.

Amesema alipopata taarifa hizo alishirikiana na jeshi la polisi kumchukua  na kumpeleka hospitalini kwa uchunguzi na uangalizi, huku juhudi za kumtafuta mama yake zikiendelea bila mafanikio.

Rais Dk. Samia amemkaribisha mtoto huyo katika familia yake na kuahidi kumpa malezi, ulinzi na huduma zote muhimu ili akue katika mazingira salama na yenye upendo.

“Wanaotupa watoto hawajui wanalolifanya. Kuliko kumtupa mtoto ni afadhali ukamkabidhi katika mamlaka za kisheria au kituo cha kulelea watoto. Kila mtoto aliyezaliwa ni hazina na hatuijui kesho yake,” amesema Rais Dk. Samia.

Previous Post

SINGIDA, SIMBA BALAA ZITO LEO

Next Post

MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

Next Post
MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

11 months ago
MSAMAHA WA RAIS DK. SAMIA WAGUSA WAFUNGWA WAZEE, WENYE UJAUZITO

MSAMAHA WA RAIS DK. SAMIA WAGUSA WAFUNGWA WAZEE, WENYE UJAUZITO

9 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA NI KIONGOZI WA MATOKEO

    RAIS DK. SAMIA NI KIONGOZI WA MATOKEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?