• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AUNGWA MKONO ULINZI WA RASILIMALI ZA NCHI 

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 2, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AUNGWA MKONO ULINZI WA RASILIMALI ZA NCHI 
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MAIGALA

BAADA ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwataka Watanzania kulinda mali za umma na kueleza uwajibikaji si chaguo ila ni wajibu, wadau mbalimbali wakiwemo wasomi, wanasiasa na viongozi wa dini wamempongeza kwa kauli hiyo na kusema hakuna maendeleo pasipo na uwajibikaji mzuri.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na UHURU, wadau hao walisema uwajibakaji unaliletea taifa maendeleo na kuondoa changamoto zinazolikabili.

KATE KAMBA

Mwanasiasa mkongwe nchini Kate Kamba alisema, uwajibakaji katika shughuli mbalimbali unaleta usawa wa maendeleo.

Kamba alisema jamii na watumishi wa umma wafuate nyayo za Rais Dk. Samia anavyowajibika katika utendaji wake wa kazi bila ya ubaguzi wowote.

“Tunamuona Rais Dk.Samia anavyowajibika kwa Watanzinia bila ya kujali dini, kabila na jinsia,”alisema.

Kamba alisema mtumishi akifanya kazi zake inavyostahili hata maendeleo ya nchi yataonekana.

DK. RUGEIHYAM

Kwa upande wake mtaalamu wa Somo la Hisabati kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Silvester Rugeihyam, aliwaomba Watanzania waige nchi zilizoendelea.

Dk. Rugeihyam alisema kuna nchi nyingi zimeendelea kwa sababu ya kujituma kwa kuwajibika.

“Tunashuhudia nchi nyingi zimeendelea kwa sababu ya uwajibikaji mzuri katika shughuli zao za kujiongezea kipato,” alisisitiza.

Alisema uwajibikaji unaendana na uwajibishwaji hivyo, viongozi wa umma wajijengee tabia ya kuwajibisha watumishi wanaofanya ubadhirifu wa mali za umma.

“Hadi leo kuna baadhi ya watumishi wa umma wanatumia vibaya mamlaka yao ya kutumia mali za umma, hivyo wanatakiwa kuwajibishwa,”alishauri.

KIONGOZI WA DINI

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT, Sheikh Alhad Mussa Salum, alisema killa mtu katika eneo lake anatakiwa kuwajibika.

Alisema wafanyakazi wa umma wanatakiwa kuihudumia jamii kwa ufanisi mkubwa.

“Ukifanya hivyo ujue huo ndio uwajibikaji, hata mimi kiongozi wa dini ninatakiwa niwajibike kwa waumini wangu kuwapa mawaidha na kuwaamrisha kutenda yale yaliyo mema,”alisema.

Sheikh Alhad alisema kuwajibika ni ibada ,kwa sababu yoyote anayewajibika ipasavyo lengo lake kwake anataka kufanya yale yaliyo mema.

AGIZO LA RAIS

Juzi alipokea Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Rais Dk. Samia aliagiza uwajibikaji wa viongozi wa umma na Watanzania kulinda mali za umma.

Previous Post

PROFESA CHIJORIGA ACHAMBUA AMANI INAVYOLETA MAENDELEO

Next Post

TRA YANG’ARA ROBO YA TATU:MAKUSANYO YAVUKA MALENGO KWA KASI YA AJABU

Next Post
TRA YANG’ARA ROBO YA TATU:MAKUSANYO YAVUKA MALENGO KWA KASI YA AJABU

TRA YANG’ARA ROBO YA TATU:MAKUSANYO YAVUKA MALENGO KWA KASI YA AJABU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA USIPIME SHINYANGA

DK. SAMIA USIPIME SHINYANGA

6 months ago
KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

KOCHA SIMBA AJITETEA, MASHABIKI WACHARUKA

3 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?