• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KOCHA SIMBA ACHEFUKWA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 11, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
KOCHA SIMBA ACHEFUKWA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

BAADA ya kushindwa kupata ushindi dhidi ya TRA United, kocha wa Simba, Steve Barker amesema kuwa amesikitishwa na kiwango walichoonesha wachezaji wake.

Pia, amesema ana kazi ya kubwa ya kufanya kupata matokeo mazuri katika michezo ijayo.

Simba juzi ilikubali suluhu dhidi ya TRA United katika mchezo wake uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Barker alisema kuwa, wachezaji wake hawakuwa na mechi nzuri juzi.

 “Sare mbili mfululizo siyo nzuri kwetu, lakini pia leo(Alhamisi) wachezaji wangu hakuwa bora, kiukweli nimesikitishwa na kiwango walichokionyesha.

“Nitapambana mwanzo mwisho kuhakikisha nafanya marekebisho katika kikosi changu tufanye  vizuri katika mechi zinazofuata,” alisema.

Barker alisema atajipanga vizuri na viongozi wenzake wa benchi la ufundi kurekebisha kasoro zote zilizojitokeza katika michezo ya hivi karibuni ambayo timu hiyo imecheza.

Aliongeza kuwa atahakikisha anafanya marekebishohasa sehemu ya ushambuliaji nafasi za kupachika mabao wazitumie vizuri.

“Tuna mechi nyingi bado, nataka kuona kikosi changu kinabadilika kiuchezaji na kuwa bora zaidi,”alisema.

Kocha huyo aliwaomba mashabiki wa timu hiyo, kutokata tamaa na kuwataka waendelee kuwapa sapoti ya kutosha kuwaongezea morari wachezaji wake wafanye vizuri.

Naye kocha wa TRA United, Ettiene Ndayiragije, alisema kuwa walicheza katika mchezo huo, kupata ushindi lakini bahati haikuwa yao.

Ndayiragije aliipongeza timu ya Simba kwa kuwapa mechi ngumu, lakini ameridhishwa na maendeleo ya kikosi chake.

“Sisi leo(Alhamisi) tulistahili kupata ushindi katika mchezo huu, lakini niwapongeze Simba kwa kutupa mechi ngumu, kikosi changu kwa sasa kimezidi kuwa bora na tutahakikisha tunafanya vizuri mechi zinazofuata,” alisema Ndayiragije.

Katika msimamo wa Ligi Simba ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 36 huku TRA United ikishika nafasi ya saba na kujizolewa pointi 24 baada ya wote kushuka dimbani mara 18.

Previous Post

NYOTA YANGA WAPEWA TANO

Next Post

CHOBWEDO ATIKISA

Next Post
CHOBWEDO ATIKISA

CHOBWEDO ATIKISA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

5 months ago
AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA

AHUKUMIWA KUNYONGWA KWA KUTIWA HATIANI KUUA

5 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?