Na MWANDISHI WETU
KLABU ya Yanga imezidi kuwa tishio Afrika baada ya kushika nafasi 12 kwa ubora huku Simba ikiporomoka katika viwango vya ubora wa klabu Afrika.
Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Simba baada ya kutokuwa na msimu bora katika michuano ya kimataifa 2025/2026 imeporomoka.
Katika viwango vipya, Simba ipo nafasi ya 11 kwa pointi 38, ikishuka kwa nafasi sita kutoka nafasi ya tano iliyokuwa nayo mwaka jana.
Katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) msimu huu, Simba ilimaliza mkiani mwa kundi D nyuma ya Stade Malien ya Mali, Esperance ya Tunisia na Petro Luanda ya Angola.
Wakati Simba ikishuka, Yanga ipo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 35 ikizipita klabu za Wydad Casablanca, ASEC Mimosas, Orlando Pirates na TP Mazembe.
Azam FC imepanda hadi nafasi ya 38 sambamba na Singida Black Stars baada ya kuishia makundi katika Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC).




