• ePaper
Thursday, April 23, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SHILOLE AMSHUKURU RAIS DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 23, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa
0
SHILOLE AMSHUKURU RAIS DK. SAMIA
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MAIGALA

MSANII wa Bongo Fleva na Mjasiriamali, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, baada ya kusema kuwa hatawaangusha wafanyabiashara wa vyakula ‘Mamalishe’.

Pia, alisema ushiriki wake katika kongamano la Kitaifa la Umoja wa Mama na Baba Lishe Tanzania (UMALITA), lililofanyika Kituo cha Kimataifa  cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam, jana, limepandisha hadhi zao na shughuli zao kwa ujumla.

Akizungumza na UHURU , Shilole alisema Rais   Samia ni kiongozi mbunifu mwenye nia ya kuwapa faraja wafanyabiashara wadogo na kutaka wakue kiuchumi.

“Rais  Samia anajua changamoto za mama na babalishe  na ndio maana ameahidi kuwa nao beba kwa bega, kuhakikisha wanafanya shughuli zao katika mazingira yaliyo bora,” alisema Shilole.

Aliongeza kuwa, kauli hiyo aliitoa Rais kuwa hatowaangusha imeleta  faraja kubwa na kuwapa nguvu zaidi ya kufanya kazi pamoja na changamoto nyingi.

Msanii huyo alisema amefurahi kushiriki kongamano ushiriki wake katika kongamano hilo ni kutaka kuona kila kitu kinaenda sawa kwa baba na mamalishe.

“Tunachangamoto nyingi katika kazi zetu hasa za kufukuzwa mara kwa mara na askari wa jiji katika sehemu tunazofanyia biashara, hukusanya vyakula na vyombo na kuondoka navyo na kutuacha tukiwa hatuna mitaji wala vyombo vya kupikia,” aliongeza.

Hata hivyo, Shilole alisema kwa kuwa tayari baadhi ya kero wamezitoa kwa Rais, anaamini mambo yatakuwa sawa.

Juzi Rais Dk. Samia alisema hatawaangusha mama na babalishe kutokana na mchango wao mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Alisema kundi hilo ni muhimu katika jamii, hivyo ataboresha kazi zao na kutatua changamoto zinazowakabili ili wafanye kazi kwa ufanisi na kukuza uchumi wa nchi.

Previous Post

DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

Next Post

‘KNOCKOUT YA MAMA’ KUWAVUTA MABONDIA KIMATAIFA

Next Post
‘KNOCKOUT YA MAMA’ KUWAVUTA MABONDIA KIMATAIFA

‘KNOCKOUT YA MAMA’ KUWAVUTA MABONDIA KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

7 months ago
KIKWETE AWATOLEA UVIVU WAZUSHI, ASEMA UTEUZI WA DK. SAMIA ULIFUATA KATIBA YA CCM

KIKWETE AWATOLEA UVIVU WAZUSHI, ASEMA UTEUZI WA DK. SAMIA ULIFUATA KATIBA YA CCM

8 months ago

Popular News

  • NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    NDEJEMBI ATAJA VIPAUMBELE 10 SEKTA YA NISHATI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU ATOA MAAGIZO ALAT

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIPOTI YA KUPONYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANDAAJI MISS WORLDTZ AITAJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, MAFUNZO HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?