• ePaper
Thursday, May 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 15, 2026
in Habari, Kitaifa
0
SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI
0
SHARES
15
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba amesema mfumo wa kidijitali wa kutoa huduma za mafuta na gesi wa PRIS uliozinduliwa na Puma Energy Tanzania ni hatua muhimu katika kuimarisha uchumi wa kisasa unaotegemea teknolojia ndani ya sekta ya mafuta nchini.

Salome alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa mfumo huo uliofanyika katika Johari Rotana jijini Dar es Salaam.

Amesema sekta ya nishati ni mhimili muhimu wa uchumi wa taifa, hivyo matumizi ya mifumo ya kidijitali yataongeza ufanisi wa utoaji wa huduma pamoja na kukuza matumizi ya teknolojia nchini.

Kwa mujibu wa Salome, mfumo wa PRIS ni teknolojia ya kisasa itakayosaidia kusimamia shughuli za vituo vya mafuta ikiwemo mauzo, malipo, usimamizi wa stoo za mafuta na upatikanaji wa taarifa za biashara kwa wakati halisi.

Amesema mfumo huo unalenga kuongeza ufanisi, uwazi na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wateja sambamba na kuboresha usimamizi wa biashara ya mafuta nchini.

Aidha, ameipongeza Puma Energy Tanzania kwa kuendelea kuwekeza nchini kupitia ubunifu wa kidijitali, upanuzi wa vituo vya mafuta na uwekezaji katika nishati safi ya CNG.

Salome alisema mfumo huo unaendana na malengo ya Tanzania ya kujenga uchumi wa kidijitali kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na mkakati wa DESF 2024–2034.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Fatma Abdallah alisema kutambulishwa kwa mfumo huo ni hatua muhimu katika safari ya kampuni ya kuendelea kuboresha huduma kwa wateja kwa kuwekeza katika suluhisho la kisasa lenye kuleta thamani halisi nchini.

Amesema kampuni hiyo ni mshirika mkubwa wa maendeleo ya sekta ya nishati nchini, ikiwa na zaidi ya vituo 100 vya huduma kote nchini, pamoja na huduma za mafuta ya ndege katika viwanja vya ndege, nishati safi ya kupikia ya Puma Gas na uwekezaji katika miundombinu ya kisasa.

“Mafanikio ya kweli huanza na mteja. Ndiyo maana leo tunazindua PRIS, programu ya kwanza nchini Tanzania inayowezesha wateja kupata huduma za Puma pamoja na zawadi mbalimbali kupitia matumizi ya mafuta na bidhaa za Puma,” alisema Fatma.

Ameongeza kuwa kupitia mfumo huo, kila mteja atakayenunua mafuta katika vituo vya kampuni hiyo ataweza kukusanya alama na kuzitumia baadaye kupata manufaa ndani ya mtandao wa kampuni pamoja na washirika wake.

Fatma amesema uzinduzi huo unaunga mkono Dira ya Taifa ya kujenga uchumi wa kidijitali unaolenga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha teknolojia ya kidijitali katika ukanda wa Afrika.

Aidha, amesema mfumo huo tayari umepata mafanikio makubwa katika masoko mengine ya Afrika ambako kampuni hiyo inaendesha shughuli zake, ikiwemo Malawi, Zimbabwe na Botswana, na kwamba hali hiyo inatoa matumaini makubwa kwa Watanzania kunufaika na ubunifu huo.

Previous Post

MTIFUANO MKALI NNE BORA LIGI KUU TANZANIA BARA

Next Post

TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

Next Post
TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

HERSI ACHOMOZA FIFA

HERSI ACHOMOZA FIFA

5 months ago
KAULI UN YAWAKOSHA MABALOZI, WAHADHIRI

KAULI UN YAWAKOSHA MABALOZI, WAHADHIRI

5 months ago

Popular News

  • MWANZO, MWISHO SIMULIZI MAUAJI YA MCHINA DAR

    MWANZO, MWISHO SIMULIZI MAUAJI YA MCHINA DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUDUMISHA SERA YA CHINA MOJA NA KUIMARISHA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIO USIPIME KABISA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA TABASAMU WAPIGANAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?