• ePaper
Thursday, May 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

RIO USIPIME KABISA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 21, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
RIO USIPIME KABISA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MUSSA YUSUPH
DODOMA

SHANGWE zimetawala katika Jiji la Dodoma na viunga vyake baada ya ujio wa mwanasoka maarufu duniani, Reo Ferdinand, aliyewahi kusakata kabumbu katika klabu ya Manchester United na Timu ya Taifa ya Uingereza.

Mchezaji huyo ambaye amefanikiwa kushinda mataji sita ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na moja la Klabu Bingwa Ulaya, aliwasili jana jijini hapa akitokea Dar es Salaam.

Baada ya kuwasili katika Stesheni ya Samia Suluhu Hassan, Ferdinand alipokelewa kwa shangwe na mamia ya wananchi wakiongozwa na kikundi maarufu cha ngoma ya asili cha Nyota.

Wakati kikundi hicho kikitumbuiza kwa nyimbo za kabila la kigogo, Rio alitoa simu yake na kuanza kurekodi hali iliyoonyesha kuwa alikoshwa na burudani iliyoporomoshwa.

Saa sita mchana, mwanasoka huyo ambaye pia ni mchambuzi wa soka, aliwasili katika viwanja vya Bunge akiwa katika gari aina ya Toyota LandCruiser V8 lenye namba za usajili T. 758 EMJ na kupokelewa na mwenyeji wake, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda.

Makonda alisema baada ya ziara hiyo mkoani hapa, staa huyo atapata fursa kutembelea ujenzi wa uwanja wa AFCON uliopo Arusha na Hifadhi ya Taifa Serengeti.

“Tumeona ni muhimu akanyaje ardhi ya Arusha ashuhudie Rais Samia anavyowekeza kwa vijana kupitia soka,” alibainisha.

Staa huyo wa soka pia alipata fursa ya kuzungumza machache na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Profesa Paramagamba Kabudi.

Katika mazungumzo hayo nje ya viwanja vya Bunge, Profesa Kabudi alimweleza kwa ufupi namna ambavyo Rais Samia amekuwa mstari wa mbele kuboresha mchezo wa soka nchini.

Pia, alimweleza kuwa akifika Serengeti atashuhudia vivutio vya kila aina ambavyo vinapatikana kwenye hifadhi hiyo.

“Ukifika Serengeti utashuhudia vivutio vyote vya uhifadhi vilivyopo Afrika katika eneo moja,” alisisitiza Profesa Kabudi.

Alisema Tanzania ni taifa lenye mchanganyiko wa  tamaduni kwa sababu ya muingiliano wa watu mbalimbali. “Tunasema kwamba Tanzania ni ardhi ya Kilimanjaro, Serengeti na Zanzibar,” alisisitiza.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AWAPA TABASAMU WAPIGANAJI

Next Post

SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

Next Post
SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMBASC INATOBOA HAPA KIMATAIFA

SIMBASC INATOBOA HAPA KIMATAIFA

6 months ago
HESABU KALI SIMBA,YANGA ZIKIWAWINDA AL AHLY, ESPERANCE

HESABU KALI SIMBA,YANGA ZIKIWAWINDA AL AHLY, ESPERANCE

4 months ago

Popular News

  • KUDUMISHA SERA YA CHINA MOJA NA KUIMARISHA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA

    KUDUMISHA SERA YA CHINA MOJA NA KUIMARISHA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIO USIPIME KABISA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA TABASAMU WAPIGANAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA SIMBA KICHEKO  

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?