• ePaper
Wednesday, April 22, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 16, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amefichua kuwa ana kipaji cha kucheza soka na wakati yupo shuleni alikuwa akisakata mpira wa miguu.
 
Dk. Mwinyi aliyasema hayo alipozungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Ikulu, Zanzibar.
 
Alisema majukumu ya taaluma ya udaktari na baadaye nafasi ya Urais yamechangia kumfanya asiendelee kushiriki mchezo huo kwa muda mrefu, licha ya kuendelea kuwa na mapenzi makubwa na mpira wa miguu.

Dk. Mwinyi alisema alipokuwa akisakata soka, alikuwa mchezaji mwenye kipaji kizuri.

“Mimi nilivyokuwa shule nilikuwa mchezaji wa mpira wa miguu na nilikuwa mchezaji mzuri sana, lakini baada ya kuingia katika maswala ya kazi haya toka niingie katika maswala ya udaktari nilikuwa nashughulika sana na kazi, kwa hiyo nikaacha muda mrefu na baada ya hapo nikaingia kwenye siasa muda haukupatikana kabisa, lakini mara moja moja tukiwa bungeni nilikuwa ninacheza,”  alisema.

Kuhusu kuhusishwa na ushabiki wa klabu ya Simba au Yanga, Dk. Mwinyi alisema hajawahi kujitambulisha kuwa upande wowote.

Amesema mara nyingi amekuwa akiulizwa kuhusu timu anayoishabikia, lakini hajawahi kuweka wazi msimamo wake, akisisitiza kwa utani kuwa, “katika hilo wamenitafuta sana hawajanipata, na wewe leo hunipati.” Dk. Mwinyi alimwambia mwandishi wa TBC huku akitabasamu.

Previous Post

PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

Next Post

YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

Next Post
YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS WA MUZIKI AHIMIZA AMANI

RAIS WA MUZIKI AHIMIZA AMANI

2 weeks ago
SIKU 100 ZA KAZI NA UTU

SIKU 100 ZA KAZI NA UTU

2 months ago

Popular News

  • YANGA YATIMUA VUMBI CAF, SIMBA MMH

    YANGA YATIMUA VUMBI CAF, SIMBA MMH

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AMPA TANO SIMBU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?