Na MWANDISHI WETU
WAAFRIKA hivi sasa wanaendelea kupata huduma mbalimbali kuhakikisha wanapunguza pengo la kidijitali na kuchochea utunzaji wa mazingira kupitia nishati safi.
Katika ripoti ya Maendeleo ya 2026, inayobainisha mafanikio yaliyopatikana katika kupanua huduma za mawasiliano, inaonesha jinsi uwekezaji wa Airtel Afrika katika miundombinu ya kidijitali, huduma za kifedha kupitia simu za mkononi, pamoja na ushirikiano wa kimkakati, ulivyoendelea kubadilisha maisha ya watu na kufungua fursa za kiuchumi na kijamii kwa jamii ambazo bado hazijafikiwa kikamilifu na huduma hizo, hususan katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Akizungumzia ripoti hiyo, Mtendaji Mkuu wa Airtel Afrika, Sunil Taldar, alisema:
”Barani Afrika, upatikanaji wa mawasiliano, huduma za kifedha na elimu ya kidijitali unazidi kuwa muhimu katika kufungua fursa za kiuchumi. Airtel Africa inaendelea kupanua huduma hizi kwa mamilioni ya watu, hususan katika maeneo ya vijijini na yale ambayo bado hayajafikiwa kikamilifu.”
“Katika mwaka huu, tumeendelea kupanua huduma za mtandao, kuongeza matumizi ya simu janja na kuimarisha huduma za Airtel Money, sambamba na kuendeleza ushirikiano wa kimkakati unaochangia mafanikio ya shughuli zetu,”.
Alisisitiza, maendeleo hayo yameendelea kuwa sehemu muhimu ya mkakati wao wa kukuza biashara na kutoa huduma bora kwa wateja. Aidha, kwa kuboresha matumizi ya nishati na kupunguza utegemezi wa dizeli, kuimarisha ufanisi na ustahimilivu wa shughuli mbalimbali za kukichangia ukuaji endelevu wa biashara na jamii.



