Na MWANDISHI WETU
TIMU ya taifa ya Mexico imeanza kwa kishindo katika Kombe la Dunia baada ya kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Afrika Kusini.
Mexico ilipata ushindi huo katika mtanange wa ufunguzi uliopigwa Uwanja wa Mexico City, Mexico.
Mabao ya Mexico yalifungwa na Quinones dakika ya tisa na Raul Jimenez dakika ya 67.
Katika mtanange huo, zilitoka kadi tatu nyekundu, mbili kwa Afrika Kusini na moja kwa Mexico.
Wachezaji wa Afrika Kusini waliopata kadi nyekundu ni Sithole na Zwane wakati wa Mexico ni Montes.
Nyota hao walipata kadi kwa muda tofauti kutokana na sababu za mbalimbali.
Mexico ndiyo kinara wa kundi A la michuano hiyo ikiwa na pointi tatu.




