• ePaper
Saturday, June 13, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 12, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI timu za Simba na Yanga zikitarajiwa kushuka dimbani wikiendi hii, timu hizo zinaingia uwanjani zikiwa kivingine huku kila upande ukitamba kuchukua alama tatu katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.

Michezo ya ligi hiyo, inatarajiwa  kuendelea  tena baada ya mapumziko ya wiki mbili huku kila timu ikipambana kuondoa kasoro zilizojitokeza  katika mechi zilizopita.

Yanga inatarajiwa kuwa ugenini kesho kupambana na Mashujaa FC katika Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma huku Simba ikishuka dimbani keshokutwa katika mchezo wake dhidi ya Pamba Jiji utakaochezwa Uwanja wa Meja Isamuhyo ikitaka kuendelea kuongoza michuano hiyo.

Akizungumza kuelekea katika mechi tano zilizobakia, kocha wa Yanga Abdihamid Moalin alisema timu yao inakuja kivingine kwa kupanga kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi zote zilizobakia wakianza na Mashujaa FC.

 “Sisi kila mchezo ni kama fainali, wiki mbili za mapumziko tumepata nafasi ya kufanya marekebisho mapungufu yaliojitokeza ili kutimiza malengo tuliojiwekea. Pia tunajua tunaenda kupambana na Mashujaa ambayo ni timu bora na yenye wachezaji wazuri,” alisema Moalin.

Naye kocha wa Simba, Steve Barker alisema ana imani kubwa na timu yake kwa mechi tano zilizobakia kupata pointi tatu katika kila mchezo.

Barker alisema hawataki kuona wanapoteza mchezo wowote ule kwani malengo yao ni kuhakikisha wanabeba taji la ubingwa msimu huu wakianza na Pamba Jiji ambayo alisema siyo timu ya kuibeza.

“Malengo yetu ni kupata pointi tatu katika kila mchezo, hatutakubali kupoteza mchezo wowote ule uliokuwa mbele yetu hivyo tutahakikisha tunapambana kwa jasho na damu ili kupata ushindi,” alisema Barker.

Hata hivyo Barker alisema kuwa amefanya marekebisho katika kikosi chake ili kuweza kufanya vizuri.

Hadi sasa Yanga imebaki na mchezo dhidi ya Yanga ikibaki na mchezo dhidi ya Mashujaa FC, Fountain Gate FC, Azam FC, TRA United na JKT Tanzania huku Simba imebaki na mechi dhidi ya Pamba Jiji, Mbeya City, Mtibwa Sugar, Singida Black Stars na KMC.

 Yanga inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 60 ikifuatiwa na Simba yenye pointi 58 huku Azam ikishika nafasi ya tatu na pointi 52.

Previous Post

MEXICO YAANZA KWA KISHINDO WC, KADI ZATEMBEA HATARI

Next Post

MWAKINYO AOMBA RADHI

Next Post
MWAKINYO AOMBA RADHI

MWAKINYO AOMBA RADHI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

9 months ago
DK. NCHIMBI ATAJA SULUHU FOLENI DAR

DK. NCHIMBI ATAJA SULUHU FOLENI DAR

8 months ago

Popular News

  • AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO AOMBA RADHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MEXICO YAANZA KWA KISHINDO WC, KADI ZATEMBEA HATARI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MWENDO WA KIDIGITALI, SUKARI SASA KUCHANGIA BIMA YA AFYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?