• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA AWAGUSA WENGI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 28, 2025
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA AWAGUSA WENGI

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Happiness Mtweve,
Dodoma

UAMUZI wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kutoa msamaa kwa vijana waliohusika kwa kufuata mkumbo katika vurugu zilizotokea Oktoba 29 mwaka huu, umepongezwa baada ya serikali kuanza utekelezaji wake ambapo watu zaidi ya 1,000 wanatarajiwa kupata msamaa huo.

Kwa mujibu wa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Juma Homera, amesema mchakato wa kuwaachia huru watuhumiwa hao unaendelea ambapo jumla ya watu 1,736 kati ya 2,045 waliokamatwa wanatarajiwa kuachiwa baada ya taratibu zote za kisheria kukamilika. 

Dk. Homera aliyasema hayo alipotembelea Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa madhumuni ya kujionea utendaji kazi na hatua zinazoendelea katika usimamizi wa mashtaka nchini jijini hapa.

“Hadi kufikia Novemba 25, 2025, jumla ya watuhumiwa 607 kati ya 1,736 wanaotakiwa kuachiwa, tayari wameachiwa huru na wengine waliobaki wataendelea kuachiwa baada ya upekuzi wa kina wa kuridhisha kukamilika,” alieleza.

Amefafanua kuwa watu 309 kati ya 2,045 waliokamatwa kazi ya ufuatiliaji inaendele ambapo alitaja mikoa na idadi ya watu walioachiwa huru ni Manyara mmoja, Mwanza 164, Dar es Salaam 263, Rukwa 10, Mbeya 69, Shinyanga wawili, Geita 74 na Arusha 24 ambao jumla ni 607.

“Tuchukue nafasi hii kumshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa hiki alichokifanya. Huu ni upendo kwa sababu yeye kama mlezi na mzazi ameamua kuchukua hatua kama hizo,”amesisitiza.

MAONI YA WANANCHI

Wakizungumzia uamuzi wa kuachiwa huru watuhumiwa hao, baadhi ya wananchi mkoani hapa wameeleza namna walivyoguswa na hatua hiyo.

Mkazi wa Chidachi, Annastazia Malegesi, amesema hatua hiyo imeonyesha dhamira ya dhati ya Dk. Samia kutaka wananchi wake waishi kwa amani na upendo.

“Tunajua wapo walioingia katika changamoto hiyo kwa kufuata mkumbo. Wengi vijana wetu hawakujua mipango mibaya ya watu kutaka kuichafua nchi yetu. Vurugu zimeichafua nchi yetu ambayo imekuwa yenye amani na utulivu kwa muda mrefu.

Amesisitiza: “Tunaomba vyombo vya dola kuendelea kuimarisha usalama wa nchi yetu kwani wapo watu wenye nia mbaya ambao hawapaswi kupewa nafasi kwa sababu ndiyo wamekuwa wakiwarubuni vijana wetu kuingia katika matatizo.”

Naye, Mkazi wa Mpunguzi, Amos Lichelile amesema Rais Dk. Samia ni kiongozi mwenye mapenzi ya dhati kwa wananchi wake na ndiyo maana mara zote amekuwa akisisitiza umoja, amani na mshikamano nchini.

Ameeleza kuwa, upendo wa Rais Dk. Samia kwa wananchi wake ndiyo sababu ya kuchukua uamuzi wa kuwasamehe vijana waliojikuta katika mikono ya dola wakati wa vurugu.

“Ninawaomba Watanzania wenzangu tukajifunze katika mataifa mengine ambayo yalikuwa yenye neema lakini sasa yameangukia katika umaskini wa kutupwa. Ukienda Libya na Sudan zilikuwa nchi zenye neema lakini sasa  hazikaliki kwa sababu ya vita.

“Walichonganishwa kwa sababu ya rasilimali zilizopo, wakakubali kutumbukia katika vita ambavyo hadi leo amani wanaisikia tu. Tusikubali kugeuzwa mfano mbaya, Tanzania ni yetu kwani ikichafuka hakuna tutakapokimbilia,” amesisitiza.

Previous Post

SIMBA SC YAWATOA HOFU MASHABIKI KUHUSU BAJABER

Next Post

SERIKALI YAWEKA BAYANA KILICHOJIRI BUNGE LA EU

Next Post
SERIKALI YAWEKA BAYANA KILICHOJIRI BUNGE LA EU

SERIKALI YAWEKA BAYANA KILICHOJIRI BUNGE LA EU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

HERSI ACHOMOZA FIFA

HERSI ACHOMOZA FIFA

4 months ago
UBINGWA LIGI KUU WAWATEGA BARKER, PEDRO 

UBINGWA LIGI KUU WAWATEGA BARKER, PEDRO 

1 month ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?