• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TANZANIA YATAJWA KINARA AFRIKA MAPAMBANO USUGU WA VIMELEA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 4, 2025
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
TANZANIA YATAJWA KINARA AFRIKA MAPAMBANO USUGU WA VIMELEA

MAKAMU wa Rais, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi.

0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI

TANZANIA imetajwa kuwa moja ya nchi kinara barani Afrika katika mapambano dhidi ya Usugu wa Vimelea vya Magonjwa Dhidi ya Dawa.

Hilo limebainishwa katika ufunguzi wa Maadhimisho ya Kanda ya Afrika ya Wiki ya Kimataifa ya Uelewa wa Kudhibiti Usugu  wa Vimelea vya Magonjwa Dhidi ya Dawa (WAAW), uliofanywa na Makamu wa Rais, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika ufunguzi huo, Dk. Nchimbi, alisema Tanzania haijajipambanua tu kama mwenyeji wa tukio hilo barani Afrika, bali mshirika muhimu na kiongozi wa kimkakati katika kukabiliana na tishio hilo.

 “Usugu wa dawa siyo jambo la baadaye, bali la sasa na matokeo yake, yanaonekana duniani kote, afya ya binadamu, wanyama, kilimo na mazingira, vimeunganishwa kwa karibu na tatizo hili, hivyo suluhisho lazima liwe la pamoja na sekta zote,”alisema.

Dk. Nchimbi, alieleza Tanzania imeweka UVIDA katika usimamizi wa kipaumbele cha taifa kwa kutekeleza Mpango wa Pili wa Taifa wa Kupambana na UVIDA (2023–2028) kupitia muunganiko wa sekta mbalimbali.

Alisema mpango huo, umeleta mafanikio makubwa ikiwemo kupungua kwa vifo, vinavyohusiana na UVIDA kwa asilimia 14.

Pia, alitaja kupungua kwa matumizi ya viuavijasumu nchini kwa asilimia 88 kama moja ya hatua za kihistoria zilizotambuliwa kimataifa na mchango wa Tanzania katika kushirikisha data za UVIDA katika majukwaa ya kikanda na kimataifa na kuongeza fedha za ndani kwa utekelezaji wa mpango huo.

Dk. Nchimbi, alisema katika kuongeza uelewa wa umma, Tanzania imeitafsiri rasmi dhana ya AMR kuwa Usugu wa Vimelea vya Magonjwa Dhidi ya Dawa (UVIDA) na imeendesha kampeni nyingi za kitaifa kuanzia ngazi ya juu hadi vijijini.

Aliitaja kampeni ya “Holelaholela Itakukosti” kama mfano bora uliotambuliwa na Afrika CDC, baada ya kufikia watu milioni 24.7.

Pia, alisema Tanzania imeanzisha ushirika wa wabunge wa kupambana na UVIDA, unaolenga kuimarisha nguvu ya kisheria, sera na ushirikiano kati ya watunga sera na wadau wa afya, mazingira, mifugo na kilimo.

Katika kukabiliana na maambukizi, alibainisha kuwa, utekelezaji wa kanuni za Kinga na Udhibiti wa Maambukizi (IPC), umeimarishwa, mifumo ya udhibiti wa usalama wa chakula, ukaguzi wa machinjio na chanjo za mifugo, imeongezwa kupunguza ueneaji wa maambukizi kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.

Dk. Nchimbi, alieleza kuwa, upatikanaji wa dawa salama, umehakikishwa kupitia mfumo wa MSD na udhibiti wa TMDA, huku Sheria ya Afya kwa Wote, ikihakikisha wananchi wanapata huduma bora bila ubaguzi.

Makamu wa Rais, alisema Tanzania imepanda kutoka kiwango cha uwezo wa chini kabisa mwaka 2016 hadi viwango vya juu vya tatu na nne kwa mwaka 2024 katika utekelezaji wa mpango wake wa UVIDA, kiashiria cha dhamira, uthabiti na uwekezaji wa muda mrefu.

Alitaja maeneo sita ya vipaumbele ambayo Tanzania itaendelea kuyaboresha ambayo ni kuongeza uelewa wa umma, kuimarisha ufuatiliaji wa UVIDA, kupanua udhibiti wa maambukizi katika hospitali na mashamba, kusimamia matumizi bora ya dawa, kuimarisha udhibiti wa sheria na kuwekeza katika utafiti na ubunifu.

Aliwashukuru washirika wengine kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika mapambano hayo ya kimataifa dhidi ya usugu wa dawa na kusisitiza kuwa, hakuna nchi inayoweza kupambana na UVIDA peke yake.

Alisema ushirikiano wa kikanda na duniani ni muhimu katika kubadilishana taarifa, kuunganisha sera na kuimarisha mipango ya pamoja.

Aliisisitiza jamii kufuata matumizi sahihi ya dawa, kukamilisha dozi, kuepuka matumizi holela na kuzingatia usafi na kanuni za udhibiti wa maambukizi.

Vilevile alisema Tanzania itaendelea kujenga mifumo imara ya afya, kuwekeza katika utafiti wa kisayansi na kusimamia matumizi ya dawa kwa kuwajibika kulinda afya ya watu, wanyama na mazingira.

WAZIRI MCHENGERWA

Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, alisisitiza umuhimu wa umoja wa kimataifa katika kupambana na tishio hilo linaloweza kudhoofisha matibabu ya kisasa.

Alisema Tanzania, ikiwa na mipango madhubuti ya kupambana na AMR, inaendelea kujizatiti katika kuimarisha mifumo ya afya kwa kuwekeza katika utafiti, kuimarisha mifumo ya udhibiti wa maambukizi na kuwajengea wananchi uelewa kuhusu matumizi sahihi ya dawa.

Previous Post

TANZANIA INAENDELEA KUALIKA WAWEKEZAJI – RAIS DK. SAMIA

Next Post

SIMBASC INATOBOA HAPA KIMATAIFA

Next Post
SIMBASC INATOBOA HAPA KIMATAIFA

SIMBASC INATOBOA HAPA KIMATAIFA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

DK. SAMIA ASEMA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TAYARI KULINDA NCHI WAKATI WA UCHAGUZI MKUU

7 months ago
DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

7 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?