• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MANGUNGU AFUNGUKA SIMBA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 20, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
MANGUNGU AFUNGUKA SIMBA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

SIKU moja baada ya Serikali kupitia Baraza la Michezo Taifa (BMT), kuidhinisha marekebisho ya katiba ya  Simba, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Murtaza Mangungu amesema kuwa wamepokea maelekezo na hivi sasa wanahitaji muda kuyafanyia kazi.

Msajili wa Vyama vya Michezo nchini, Abel Ngilangwa alisema miongoni mwa maboresho yaliyoidhinishwa ni kuweka wazi nafasi ya Simba Sports Club Company Limited kama chombo kitakachosimamia masuala ya kibiashara na kiutendaji, huku umiliki wa hisa ukiendelea kuwa chini ya Baraza la Wadhamini kwa niaba ya wanachama.

Pia, serikali ilibainisha kuwa muundo mpya wa Baraza la Wadhamini utakuwa na wajumbe wasiopungua watano na wasiozidi saba, watakaosimamia mali za klabu kwa niaba ya wanachama, huku Mkutano Mkuu ukiendelea kuwa chombo chenye mamlaka ya mwisho.

Akizungumza mara baada ya kuidhindishwa kwa marekebisho hayo, Mangugu alisema watakwenda kufanyia kazi haraka kulingana na kile ambacho kimewasilishwa.

Alisema mchakato wa mabadiliko ndani ya klabu hiyo unagusa mamlaka zaidi ya moja za serikali, hivyo kuna mambo mengi ambayo yanahitaji muda zaidi.

“Niwaambie kuwa tunahitaji muda kwani kuna eneo linalosimamiwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kuna eneo linalosimamiwa na Wizara ya Katiba na Sheria, pia kuna eneo linalosimamiwa na Wizara ya Viwanda na Biashara, hivyo hatuwezi kufanya kwa haraha jambo hilo ila tutalifanyika kazi,” alisema Mangungu.

Hata hivyo wadau wa mchezo wa soka, walisema kuwa hilo ni jambo zuri kwa Simba na wana imani kuwa watafanikiwa katika machakato wao huo.

Akizungumzia hilo, Kenedy Mwaisabula alisema hivi sasa wanakwenda kuwa na Simba mpya, kwani mchakato ulikuwa wa muda mrefu, wanaelekea mwishoni, hivyo anaamini na klabu zingine zinatakiwa kuiga mfano huo.

Naye aliyekuwa kiongozi wa zamani wa Simba, Hassan Hasanoo alisema wamefurahia marekebisho hayo kutoka BMT ana imani Simba inakwenda kuwa bora zaidi.

“Timu yetu bado imara na nina amini mchakato wa mabadiliko ukimalizika tutakuwa na Simba bora zaidi ya hivi sasa,” alisema Hassanoo.

Previous Post

TRA YABAINI MCHEZO MCHAFU UKWEPAJI KODI  BANDARI KAVU

Next Post

MATOKEO YAMSIKITISHA KOCHA YANGA

Next Post
MATOKEO YAMSIKITISHA KOCHA YANGA

MATOKEO YAMSIKITISHA KOCHA YANGA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ATAJA FAIDA ZA MPANGO WA NISHATI

RAIS DK. SAMIA ATAJA FAIDA ZA MPANGO WA NISHATI

2 months ago
DK. CHIMBI AFICHUA KIINI ONGEZEKO LA WAWEKEZAJI

DK. CHIMBI AFICHUA KIINI ONGEZEKO LA WAWEKEZAJI

7 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?