• ePaper
Saturday, June 6, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA ATOA MWELEKEO WA KITAIFA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 17, 2026
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA ATOA MWELEKEO WA KITAIFA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mwandishi Wetu

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza matokeo ya Tume Huru ya Uchunguzi iliyoundwa kuchunguza matukio ya Oktoba 29, mwaka, yataongoza hatua ya serikali katika uwajibikaji, maridhiano na mageuzi ya taasisi.

Pia, alisema serikali itaendelea kusimamia mchakato wa maridhiano, yakiwemo majadiliano kupitia majukwaa yaliyopo kisheria na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali.

Rais Dk. Samia alitoa msimamo huo juzi jioni, alipopokea ujumbe maalumu kutoka kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Shirley Ayorkor Botchwey, uliowasilishwa kwake na Mjumbe Maalumu, Rais Mstaafu wa Malawi, Dk. Lazarus Chakwera, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Ujumbe huo umeainisha maeneo ya kipaumbele yanayofuatiliwa na Jumuiya ya Madola, ikijumuisha uwazi na ushirikiano katika tathmini ya matukio yaliyojitokeza wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka jana na kupanua ushiriki wa kisiasa, kuendeleza majadiliano ya vyama na kuimarisha uwajibikaji wa taasisi.

Katika ujumbe wake, Shirley alisisitiza dhamira ya Jumuiya ya Madola kuendelea kushirikiana na Tanzania kuimarisha misingi ya demokrasia, utawala bora na maridhiano ya kitaifa kufuatia matukio yaliyojitokeza wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka jana.

Alisema Jumuiya ya Madola inaunga mkono juhudi zinazoendelea nchini na iko tayari kusaidia kujenga mazingira ya kisiasa yenye utulivu, ushirikishwaji na kuaminiana kupitia mazungumzo na mageuzi ya taasisi.

RAIS DK. SAMIA

Akizungumza wakati wa kupokea ujumbe huo, Rais Dk. Samia alisema Tanzania inaendelea kushughulikia hali hiyo kupitia taasisi zake, huku akitaja hatua mbalimbali zilizochukuliwa na serikali, ikiwemo kuunda Tume Huru ya Uchunguzi kurejesha utulivu na kuimarisha uwajibikaji nchini.

Alisema serikali itaendelea kusimamia mchakato wa maridhiano, yakiwemo majadiliano kupitia majukwaa yaliyopo kisheria na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali.

Kwa upande wake, Chakwera alieleza utayari wa Jumuiya ya Madola kuendelea kushirikiana na Tanzania katika juhudi za kuimarisha utawala wa sheria, ushirikiano wa kisiasa na mshikamano wa kitaifa.

Katika hatua nyingine, Chakwera, amehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tisa nchini, kama Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, kufanya tathmini ya hali ya kisiasa na mchakato wa maridhiano, ambapo alikutana na wadau mbalimbali wa siasa na taasisi za kiraia nchini

Previous Post

KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

Next Post

DK. JAKAYA AKUTANA NA RAIS RUTO JIJINI NAIROBI

Next Post
DK. JAKAYA AKUTANA NA RAIS RUTO JIJINI NAIROBI

DK. JAKAYA AKUTANA NA RAIS RUTO JIJINI NAIROBI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA : UTAKUWA UCHAGUZI WA AMANI

DK. SAMIA : UTAKUWA UCHAGUZI WA AMANI

9 months ago
SERIKALI KUANZISHA KITENGO MAALUM KUPOKEA MAONI YA WANANCHI SAA 24

SERIKALI KUANZISHA KITENGO MAALUM KUPOKEA MAONI YA WANANCHI SAA 24

6 months ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?