• ePaper
Saturday, June 6, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

SIMBA KASI ILE ILE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 20, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
SIMBA KASI ILE ILE
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

TIMU ya soka ya Simba imeendeleza kasi ya ushindi katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu baada ya jana kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Namungo.

Wekundu hao wa Msimbazi walipata ushindi huo ugenini katika Uwanja wa Majaliwa uliopo Ruangwa mkoani Lindi.

Katika mtanange huo, mabao ya Simba yaliwekwa kimiani na Libasse Gueye, Anicet Oura na Ellie Mpanzu wakati bao la Namungo likifungwa na Eliuter Makambo.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa Simba katika Ligi Kuu Bara baada ya wiki iliyopita kuifunga Fountain Gate mabao 3-0 katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.

Katika mtanange wa jana, kikosi hicho cha Kocha Steve Barker, kilimaliza kipindi cha kwanza kikiongoza kwa mabao 2-1.

Gueye alikuwa wa kwanza kuifungia Simba katika dakika ya 12 kabla ya Oura kuongeza bao la pili dakika ya 22.

Hata hivyo, dakika 12 baadaye, Namungo ilipata bao la kwanza kupitia kwa Makambo aliyefunga kwa penalti, kufuatia kiungo wa Simba, Yusuph Kagoma kushika mpira ndani ya eneo la hatari.

Kipindi cha pili, Mpanzu aliyeingia akitoka Selemani Mwalimu, alikamilisha karamu ya mabao kwa shuti la mguu wa kushoto.

Kufuatia ushindi huo, Simba inaendelea kusalia nafasi ya pili kwa pointi 42 baada ya kushuka dimbani mara 19, ikiwa chini ya kinara Yanga yenye pointi 47 katika mechi 19.

Namungo FC: Mussa Malika, Bakari Hussein, Machela Julius, Hamisi Halifa, Hamisi Mgunya, Rodgers Gabriel/Cyprian John,  Hashimu Manyanya, Heritier Makambo/Fabrice Ngoy, Abdulkarim Kiswanya na Jacob Masawe.

Simba:Mohamadou Kassali, Shomari Kapombe, Libasse Gueye, Yusuph Kagoma, Selemani Mwalimu/Elie Mpanzu, Anicet Oura, Inno Loemba/Neo Maema, Rushine De Rueck, Ismael Toure, Anthony Mligo na Clatous Chama.

Previous Post

DAKTARI ATAJA DALILI ZA SHINIKIZO LA DAMU

Next Post

RAIS DK. SAMIA ABADILI MATUMIZI YA FEDHA

Next Post
RAIS DK. SAMIA ABADILI MATUMIZI YA FEDHA

RAIS DK. SAMIA ABADILI MATUMIZI YA FEDHA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NEEMA YA AJIRA MAMBO YA NDANI

NEEMA YA AJIRA MAMBO YA NDANI

2 weeks ago
WASIRA AONYA WANAOTOLEA MACHO UMEYA

WASIRA AONYA WANAOTOLEA MACHO UMEYA

8 months ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?