• ePaper
Saturday, June 13, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MWAKINYO AOMBA RADHI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 12, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
MWAKINYO AOMBA RADHI
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

AMINA KASHEBA

BONDIA nyota wa Tanzania, Hassan Mwakinyo ameomba radhi kwa mashabiki wake kufuatia kupoteza pambano la kuwania mkanda wa Ubingwa wa Dunia  (IBO) dhidi ya Michel Soro kutoka Ufaransa.

Mwakinyo alishindwa kutwaa mkanda huo baada ya kupoteza kwa Technical Knockout (TKO) katika raundi ya tisa ya pambano la raundi 12, uzito wa kati ambalo lilitarajiwa kuwa moja ya mapambano makubwa katika safari yake ya ngumi za kulipwa, lililofanyika nchini Ivory Coast.

Akizungumza baada ya kumalizika pambano hilo, Mwakinyo alitoa pole kwa mashabiki wote walioumizwa na matokeo hayo, kwani kushinda na kushindwa ni sehemu ya mchezo.

Alisema kilichomuumiza zaidi si kupoteza pambano hilo, bali kushindwa kuonyesha kiwango chake halisi kutokana na kuwa katika hali ya udhaifu ambayo ilimfanya ashindwe kujitetea ipasavyo ulingoni.

“Siuumii kwa sababu ni mchezo, lakini kinachoniumiza ni kuwa dhaifu kiasi cha kushindwa kuonyesha upiganaji wangu wa kawaida, hiyo ndiyo sababu kubwa ya masikitiko yangu,” alisema Mwakinyo.

Mwakinyo alisema maandalizi yake yalikuwa mazuri na alifanya mazoezi makali ya nguvu kwa lengo la kuhakikisha anapata ushindi, lakini hali ya mwili wake siku ya pambano haikuruhusu kutoa kile ambacho mashabiki wamezoea kukiona kutoka kwake.

“Nimeyapokea matokeo haya narudi kujipanga upya kwani nitakuwa nipo imara zaidi katika mapambano yajayo, “ alisema Mwakinyo.

Matokeo hayo yanaifanya rekodi ya Mwakinyo kupata pigo jingine katika ngumi za kulipwa, huku Soro akiendelea kuthibitisha ubora wake katika medani ya kimataifa.

Wadau wafunguka

Promota wa ngumi za kulipwa, Ernest Evarist ‘Mopao’ alisema bado Mwakinyo ana muda wa kurekebisha kasoro zilizojitokeza kabla ya kupanda ulingoni katika mapambano mengine.

 “Muda bado upo wa kufanya uboreshaji nina imani Mwakinyo ana nafasi ya kuonyesha uwezo wake, watanzania wanapaswa kufahamu mchezo wa ngumi una matokeo matatu,” alisema.

Bondia, Twaha Kassim ‘Twaha Kiduku’ alimpa pole Mwakinyo na kumtaka ajipange upya kwa ajili ya kufanya vyema katika mapambano mengine.

“Pole kwa Mwakinyo kwa kupoteza hili siyo jambo geni kwani utokea kwa mtu yoyote, muhimu anapaswa kujipanga upya na kuangalia wapo ameanguka,” alisema Twaha Kiduku.

Naye bondia, Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’ alisema matokeo ya juzi hayawezi kushusha kiwango na juhudi za Mwakinyo hivyo ana imani atafanya vyema wakati mwingine.

“Ninaamini bado una uwezo mkubwa, matokeo ya leo hayawezi kufuta juhudi na kipaji chako  wapongeza wote waliocheza leo wameonesha mchezo mzuri japo bahati haikuwa kwetu,” alisema Dullah Mbabe.

Previous Post

YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

Next Post

AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

Next Post
AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

7 months ago
TUME ILIYOUNDWA NA RAIS DK. SAMIA ILIVYOBEBA MATUMAINI YA AMANI

TUME ILIYOUNDWA NA RAIS DK. SAMIA ILIVYOBEBA MATUMAINI YA AMANI

2 months ago

Popular News

  • AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO AOMBA RADHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MEXICO YAANZA KWA KISHINDO WC, KADI ZATEMBEA HATARI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MWENDO WA KIDIGITALI, SUKARI SASA KUCHANGIA BIMA YA AFYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?